Author :Dr. Omar Khatib
Date:Sun, 19 Dec 99
Subject: UGONJWA WA KISUKARI
_____________________________________________________
Assalaam Aleykum wanazanzinet,
Nitazungumzia somo la hapo juu yaani KISUKARI (DIABETES)
MAELEZO:
Mwezi huu wa Ramadhani unaambatana na ulaji wa vyakula vingi na vya
mchanganyiko. Vyakula vingi hivyo vimo katika aina tatu zijulikanazo kama:
UWANGA (Starch au Carbohydrates)
MAFUTA (Oils au Lipides)
Mchanganyiko wa Vitamini na madini (Vitamins na Trace Minerals)
Kila kimoja katika hivi kina kazi yake. Uwanga ndio unaleta nguvu (energy)
ya
kufanya kazi katika kila sehemu au kijisehemu cha miili yetu. Asilimia
kubwa ya
vyakula ni uwanga (carbohydrates). Mafuta nayo pia inapohitajika hutumiwa
kutoa
nguvu
lakini zaidi ndiyo inyotuletea shaham ndani ya miili yetu. Vitamini na
madini
huleta uzima wetu kwani japo mahitaji ya yake ni madogo lakini
yanahitajika
katika ujenzi na ulinzi wa miili.
Katika mwezi huu ni vigumu kuapata uiano wa vyakula hivi (balance diet) na
haitegemewi kama watu kweli wangeweza kusikia kufanya hivyo baada ya funga
ya
siku nzima na matamanio yake. Hata hivyo basi ni vyema kuelewa nini
kinatookea
baada ya mlo wa futari.
MTAFUNO WA CHAKULA (DIGESTION)
Baada ya kwisha kula na chakula kuingia ndani ya matumbo inafuata mtafuno.
Huu
ni tafauti na ule wa ng'ombe ambae hukitoa chakula matumboni na kukileta
mdomoni
na kukitafuna tena. Sisi binaadamu hatuna uwezo huo. Tumbo linatufanyia
kazi
yote hapo. Mtafuno unaotokea katika tumbo na ndani ya machango husababisha
chakula kusagwa na kuvunjwa vunjwa na kupatikana sukari aina ya GLUCOSE.
Hii ni
aina safi ya sukari ambayo inaweza kutumiwa na sehemu zote za mwili. Sasa
sukari
hiyo husafirishwa na damu kwenda katika kila sehemu ya mwili. Kama
muelewavyo
hakuna sehemu ya mwili ambapo damu haiifikii. Kama
nilivyoeleza hapo juu sukari ndio chanzo cha mwili kupata nguvu lakini
kupatikana nguvu kunahitaji sukari itoke kwenye damu na iingie kwenye
misuli au
chembe za mwili (body-cells) na huko sukari ivunjwe kwa kutumia hewa ya
OXYGEN
iliipatikane nguvu.Sukari hutoolewa kwenye damu kwenda huko kwenye misuli
na
chembe za mwili kwa kutumia chemikali ya INSULIN inayotemwa katika
machango na BANDAMA (PANCREASE.)
Sasa kwa wenzetu wenye kuuguwa maradhi ya KISUKARI hapa ndipo panapoleta
mushkeli wote wanapo kula vyakula vyenye sukari. Insulin inayotoka kwenye
bandama (Pancreas) zao huwa ama haitoshi kuitoa sukari yote kwenye damu na
kuipeleka
huko au huwa haipo kabisa.
Nini kitaokea mtu anapokuwa na maradhi hayo?
DALILI ZA KISUKARI
YAKUMBUKE MAMBO MATATU YAFUATAYO:
- Wingi wa kukojoa kojoa;
- Wingi wa kiu
- Wingi wa njaa
Haya ni mambo ambayo katika Ramadhani ni ya kawaida kwa kiasi fulani
lakini
jiangalie na jipeleleze na ukiwa na wasi wasi basi muone daktari umueleze
na
akufanyie uchunguzi.
AINA ZA KISUKARI
KUNA AINA MBILI MUHIMU ZA KISUKARI nazo ni:
AINA 1 = KISUKARI Kinacho tegemea INSULIN PEKEE yaani lazima kupata
INSULIN
AINA 2 = KISUKARI Kisicho tegemea INSULIN yaani inaweza kutumiwa vidonge
badala ya INSULIN
NANI ANAWEZA KUPATA KISUKARI?
WAFUATAO WANAWEZA KUPATA MARADHI YA kisukari:
- Mtu mnene mno (overweight);
- Mtu anaezidi umri wa miaka 40;
- Mtu mwenyekuhusiana na mwenye KISUKARI (nakusudia mtu ambaye
ana jamaa wenye
maradhi hayo ndani ya ukoo wake);
- Mwanamke mjamzito mwenye toto nene(large baby).
Naomba tufahamu kwamba hizi ni dalili zinazo ashiria uwezekano wakupata
maradhi
(risk factors). Ukiwa na hayo basi ni vyema ukajiangalia na ikiwezekana
kufanya
uchunguzi wa kuhakikisha hali yako ikoje.
JEE KUNA MATIBABU (CURE) YA KISUKARI?
JAWABU NI KWAMBA KWA SASA HAKUNA MATIBABU HAYO ILIOPO NI TIBA YA
KUMPUNGUZIA
MGONJWA MASHAKILI YA MARADHI HAYO.
Kwa mgonjwa wa AINA 1 atahitaji kupata tiba ya Insulin, achunguzwe damu
yake
kila mara, ale vyakula vya kisiha ambavyo havina sukari nyingi (ngano
nzima,
mtama, uwele, maharagwe, kunde, nk.) na ajishughulishe na uzoefu wa
mazoezi ya
mwili.
Kwa mgonjwa wa AINA 2 atahitaji vidonge vya matibabu, chakula chenye siha
kama
mwenziwe mwenye AINA 1 na pia afanye mazoezi. Nae pia anahitaji kuchunguza
damu
yake hasa pale anaposhindwa na ulafi wa kubwagia utamu.
Tukumbuke kwamba maradhi yo yote yale yanahitaji kugunduliwa mapema kabla
ya
kuathiri kiwili wili ili maisha yawe ya raha zaidi bila matatizo makubwa
ya
kiafya.
Tukumbuke duniani leo kuna watu zaidi ya milioni 140 wana KISUKARI idadi
huenda
ikaongezeka kufikia milioni 300 mwaka 2025.
Tujitahidi tusiwekatika hao wataoiongezea hisabu ya maradhi haya.
Tuhakikishe
UZIMA wetu.
Wenu,
Dr. Omar.
|