Author : Abdullah Abdullah
    Date: Tue, 08 Feb 2000
Subject: NCHI YETU, ZANZIBAR

Asslaaam alikum Wananeti.
Mimi ni mzanzibar ambaye sina cha kuchangia katika neti hii iliyojaa wasomi 
lakini kwa leo nawaomba kwa ihsani zenu mnisikilize.

Kila mtu anaelewa mambo yanavyokwenda nyumbani kwetu zanzibar na pengine 
kuna watu wengi wenye fikra kama zangu kuhusu matokeo ya ugomvi wa 
Wazanzibari na fursa inavyotumiwa na wenye mipango yao dhidi ya Wazanzibari.
Bila ya shaka ndugu zangu mko macho, lakini nahisi kutokana na mambo 
yaliyotuzunguka hivi sasa tuwe macho zaidi. tabia yetu ya kugombana kwa 
maslahi ya kibinafsi tuiache kwani nchi yetu inatutoka na hali tunajuwa na 
tunaiona ikiondoka. bahati mbaya ni kuwa kila wazanzibari tunapotokea 
kutofahamiana wenzetu wa bara huchukuwa fursa ya kupitisha miswada yao 
amabayo pengine ina faida ya muda mfupi lakini huwa ni kensa kwa nchi ya 
zanzibari na pale tunapokuja kuamka huwa tayari tumeshajifunga kwa sheria 
ambazo tumezipitisha wenyewe bungeni.
Mwaka 94/95 ilipitishwa mapendekezo bungeni ambayo yalimfanya Rais wetu wa 
zanzibar kuwa sio tena Makamo wa rais tanzania, Kwa nini?
hivi sasa kutokana na magazeti yasemavyo ni kuwa Rais wetu ni wa Nne 
kimadaraka ya Kitanzania. Jee hatukujuwa haya Wazanzibari? Jee ni kwa 
manufaa ya nani mapendekezo hayo yalipopitishwa? Jee nini matokeo yake hivi 
sasa? Rasi wetu amabye ilikuwa awe wa Pili kimadaraka Katika Jamhuri ya 
Muungano sasa anapotaka kutowa uamuzi imekuwa hauna nguvu kama Kiongozi 
Mshirika wa Jamhuri hii. Jee Mwenyekiti wa CCM hawezi kumuuzulu Rais wa 
zanzibar kama Mwanachama? Ikiwa anaweza jee tunasahau mambo kama hayo.

Hivi sasa mapendekezo na miswada mipya imekuja tena baada ya kuhisi kuwa 
wabunge wetu wa CCM zanzibar hawana la kuchaguwa ila kuyakubali mapendekezo 
hayo huko Bara pengine ili na wao waachiwe bila pressure kufanya mabadiliko 
huku nyumbani pia. Lakini jee ikiwa itatokea hivyo, ni nani atayekuwa 
mshindi na nani atayepata hasara ya milele. bila ya shaka ni Wazanzibari wa 
makunduchi, Chaani, Micheweni, Chake chake, Matemwe,Mzambarauni,Tumbe, 
Tumbatu na kwengineko. Jamani kwa ihsani zenu fikirieni mapinduzi yalifanywa 
kwa damu nyingi kupotea na roho za Waislam kwa lengo la kutafuta kuondowa 
madhila, uonevu, dharau, na kuwa kila mzanzibari awe huru na haki nchini 
kwake.Jee haya mapendekezo tunayoyapitisha Bungeni kila mara bila ya 
kupingwa na wazanzibari yatawaletea au kuwadumishia wazanzibari uhuru wao, 
yataondowa au yataleta tena madhila? Jee dharau  haitomfika tena mwafrika 
Mzazibari jamani? Jee madhila hayatorejea karibuni jamani? Jee uhuru wetu 
kama Wazanziari bado tunao? Jee tunao uhuru wa kuhjiamulia ndugu zangu?

Sasa ikiwa tuko tayari kupitisha kila pendekezo linaloletwa bungeni ili 
tuendelee kupata pesa za ubunge au kuogopa kusema kweli basi ndugu zangu 
Wazanzibari tujutayarishe kuwa vizazi vyetu vijavyo havitokuwa na nchi, 
uongozi, pahala pa kujidai kusema hapa ni kwetu.
ndugu zangu wazanzibari, leo wanaoathirika na hali ya kisiasa zanzibar ni 
Wapemba lakini kwa namna miswada munavyoikubali bungeni ipo hatari kwa kiasi 
kikubwa kuwa na Wazanzibari asilia watafikwa na hali kama waliyonayo wapemba 
si katika miaka ya mbali. Jee mko tayari yatokee hayao jamani?

Wazanzibari tulioko bara tunaambiwa tusijishughulishe na Siasa wakati 
wenzetu wa bara wanapokuja zanzibar hukaa miaka miwili tu na mwaka wa tatu 
akaanza kugombania uongozi na bahati mbaya tulivyokuwa hatuna uzalendo 
tunawapa uongozi na kuwaacha Waunguja na Wapemba.Jee baada ya miswada hiyo 
ijayo na myengine kufuatia baadae mnafikiri ndugu zangu tutasalimika? Jee 
wazanzibari tutakuwa na uwezo wa kusema kama Wazanzibari Bungeni? 
Wazanzibari tafadhalini kuweni kitu kimoja katika Maslahi ya nchi yetu.

Ndugu zangu wabunge wa CCM na CUF tafadhalini linapokuja suala la maslahi ya 
nchi yetu na vizazi vyetu basi tafadhalini Muungane, muwe kitu kimoja 
kuitetea sehemu yetu ya Muungano na isiwe sisi kugawiwa na kuwa dhaifu 
katika Maamuzi muhimu yanayohusu nchi yetu.
Inasikitisha sana kuwa imefika Mzanzibari kusimama mahakamani na kueleza 
kuwa zanzibar si nchi.na Rasia ni wa nne
kimadaraka.Tunagombanishwa na kutawaliwa.Kwa nini Upinzani ukae bara, 
salama,na wakati huo huo serikali ya Muungano iwe inajigamba kuwa CCM wa 
zanzibar ni wenzao? Bali upinzani upate nguvu kidogo na uweze kuisumbuwa 
serikali ya zanzibar ili wawe frustrated na miswada ifanywe na bila ya shaka 
kwa usalama wao hawatoweza kukataa. Tafadhalini tujifunze katika miswada 
iliyopita ni matokeo yake? Wabunge wetu wa CCM mkishaipitisha miswaada hiyo 
ya huko Bungeni ambayo pengine baadhi yake ni madhara kwa zanzibar 
msifikirie, hata kama mmekubaliana,kuwa Serikali ya Muungano itawakubalia 
kufanya mtakavyo Zanzibar pindi wao wakihisi hakuna maslahi kwao. Ng'o.     
kwa hiyo tusiwape nguvu zetu wakazitumia na wakati tutapotaka msaada wao 
wakatugeukia.

Jamani Wabunge wa wazanzibari (CCM na CUF) tafadhalini msigawike katika 
kuyateteya maslahi yetu bungeni kwa Muungano. Ikiwa haya ninayosema 
hamyaamini, tafadhalini tizameni mifano ya Yugoslavia na Kosovo, Yugoslavia 
na Bosnia, Tizameni sababu za Waislam kupinduliwa na kuuliwa na kufukuzwa na 
kupigwa marufuku Uislam Spain. Jee Wazanzibari mko tayari muambiwe au 
kumrishwa kuwa Adhana ni marufuku kusomwa kwa kipaza sauti? Ikiwa 
tutaendelea kugombana wenyewe kwa wenyewe hayo hayako mbali ndugu zangu.

Ndugu zangu wabunge,maisha yenu hapa ardhini ni mafupi sana na maisha ya 
baadae akhera ni marefu sana. Tafadhalini msisahau akhera zenu kwa kwa ajili 
ya ushindani wa kuwa lazima nikushinde na bora litote lakini nyinyi 
msikaribie utawala. hao mnaogombana nao ni wazanzibari wenzenu,  waisalamu 
wenzenu na after all ni jamaa na ndugu zenu. Jee bora aje kutawala mtu wa 
mbali zanzibar kuliko kutawala Mmatemwe, au Mmakunduchi au Mmicheweni, au 
Mkengeja jamani? Tafadhalini tunakuombeni sisi watoto wenu mtizame 
tunakokwenda tusiharibikiwe jamani.Kama ni makosa yaliotokea mpaka Rais wetu 
akawa hana madaraka katika Muungano, basi jamani tafadhalini tusiyarudie.

Itafika wakati nyinyi wabunge wetu leo mtakuwa wazee na sisi watoto ndio 
vijana na tutataka kuongoza nchi yetu kulingana na jamii yetu bali kwa 
sheria mnazozipitisha nyinyi leo tutashindwa kufanya hivyo na mfano wa 
karibu sana ni masuala ya zanzibar kujiunga na OIC,na zanzibar kuwa Custom 
duties na taxes wanazohisi zina maslahi kwao. Jee tumeweza?

Yako mambo mengi sana yatakuja zaidi na zaidi ikiwa hatutokuwa waangalifu 
tukashirikiana katika Mambo yanayoihusu Zanzibar. Ikiwa wewe Mbunge 
mwakilishi wa watu Wa Zanzibar Bungeni utajali Maslahi binafsi au ya chama 
chako tu bila kujali Zanzibar kama nchi au sehemu ya Muungano, nani 
atayatetea maslahi ya Wazanzibari huko.

Jamani takriban nyote muliochaguliwa Ubunge ni wasomi au watu wenye uzoefu 
katika siasa, tafadhalini msifanye mchezo na nchi yetu. Chama ni chama 
lakini nchi si chama. Na nyinyi kumbukeni nyote ni wananchi Wazanzibar.Hata 
kama utakwenda Uganda ambako pia ni Afrika utaitwa mzanzibari,ukenda kenya 
ni hayo hayo, ukinda kukaa mwanza ni hayo hayo hata kama una asili ya 
kisukuma na hutopata haki na hadhi kama watayopata wenyekuzaliwa pale. 
Jamani tusijidanganye, tunaumia. Jamani thamani ya nchi yako huwezi 
kuilinganisha na kitu chochote.Ndio utu wetu, ndio starehe, ndio uhuru, nk.

Tizameni watu kama Wapalestina walivyohangaika na mpaka leo wanapata tabu. 
popote walipo hawana raha na kwao hakurudiki.Na wanakutaka lakini wapi, 
wanakusikia tu wengine.Na wengine pamoja na raha walizokuwa nazo katika nchi 
mbali mbali ilipopatikana fura ya kurudi walirudi. Si Wapalestina tu, bali 
hata Waezraeli yaliwakuta majambo na miqasa ya nchi.Jamani mtu kwao.
Jee Wazanzibari hamjuwi kuwa "Mtu Kwao"? eeennnn!!!

Kwaherini na ahsanteni sana kwa kuisoma risala hii refu lakini naamini 
umefaidika. Nakuombeni ndugu zetu mliokaribu na walioko madarakani hivi sasa 
muwafikishie jamaa zetu ujumbe huu na ishaallah mema hauozi katu.
Atayefanya wema anaifanyia nafsi yake (ni wake huo), na ataefanya ubaya 
ajuwe kuwa uko shingoni mwake na atakutana nao duniani au mbele ya haki au 
mwote muili. Tunamuomba Mola wetu atujaaliye tuwe katika watu wanaosikiliza 
maelekezo mazuri na wakayafuata.
Ndugu yenu.
Abdul.