Author :
Hashil Seif Hashil
Date:
Mon, 17 Jan'00
Subject:
WACHENI KUBWABWAJA UKABILINI UKWELI ULIVYO
From: Hassan O. Ali
Subject: "WACHENI KUBWABWAJA UKABILINI UKWELI ULIVYO" (fwd)
---------- Forwarded message ----------
Date: Mon, 17 Jan 2000 11:19:10 +100
From: Hashil Seif Hashil
To: hassan
Subject: "WACHENI KUBWABWAJA UKABILINI UKWELI ULIVYO"
Dear Hassan O. Ali, 17.01.2000
Natumai nyote huko muliko mwabesa na kuendelea na harakati za
kimaisha za kila siku. Na sisi ndugu zenu tulioko ngambo ya pili
wazima kama chuma cha pua.
Kama ujuavyo kinapotokea chochote kile cha kutukoroga vichwa
vyetu; moyo wetu unakuwa hautupi kukaa kimya bila ya kutowa
mchango wetu japo mstari mmoja.
Kwa hivyo ningekuomba niliyonayo moyoni warushie Wazanzibari
wenzangu waoni dukuduku langu:
" WACHENI KUBWABWAJA UKABILINI UKWELI"
Nimejaribu kwa upande wangu kufatiliza huu mjadala uliopo hivi
karibuni uliochokorwa na aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa
Serikali ya Muungano Hakimu Joseph Sinde Warioba kuweza
kuikwaruza kovu kwa msumari, wakati alipotamka:" kuendelea
Dk.Salmin na wadhifa wake kwa awamu ya tatu kuwa ni kuleta
Usultani".
Msemaji wa Serikali ya (SMZ) Bw. Hafidh Ally amekuja juu mithili
ya mtu aliyetia moto kwenye pango na ndani yake alikueko nyoka
amejipumzisha wakati amesha mmeza mbuzi mzima !
Hakimu Joseph Sinde Warioba "kawatukana kistaarabu"; lakini
hawakumfahamu hata kidogo. Ole wao. Hivyo kweli Warioba hajuwi
maana ya Usultani ?.
Kwanza yeye inafaa ifahamike kuwa ni Mwanasharia na kaliangalia
jambo linalotaka kufanywa na Serikali ya Zanzibar huenda likaleta
hatari kwao na vile vile kwa Muungano wa nchi mbili yaani
Tanganyika na zanzibar.
Kubadilisha KATIBA siyo jambo la masihara hata kidogo.Kwani
katiba ni kama "uti" wa mgongo kwa mwanaadamu.Haiwezekani
hata kidogo watu kufanya utani na katiba ya nchi bila ya ridhaa ya
wananchi wote waishio kwenye visiwa hivyo.
Ukiwasikiliza kwa makini sababu zao za kutaka kuibadiliska katiba
katu haziingii akilini hata mtu akijaribu kuvuta Bangi.
Wanavyojigamba kuwa Umma wa Visiwani wanamtaka Dk. Salmin
Amour aendelee kuwa Rais wa nchi hiyo kwa sabab ya Kiuchumi
na Siasa.
" Ninani unafikiri atakaye weza kununua bidhaa hiyo
wanayoitangaza". Na akina nani hao wanaowasemea kuwa
wanamtka Dk.Salmin aendelee !!!!!!!!!
Suala liliopo hapa ni kama ifatavyo: Kwanza hawa ndugu zetu
wanaopiga makelele kama kumfanyia
kampeni Dk. Salmin Amour aendelee kutawala watufahamishe vitu
viwili kwanza. Kwani lazima ziko < skuli mbili > za kulimungunya
suala hili:
(a) Kama Dk. salmin Amour kawapa "taa ya kijani" (green Light)
wamfanyie hii kampeni wanayoifanya ya kutaka kubadilisha katiba
ili imfanye asimamie tena Urais kwa awamu ya tatu.
(b) Au wanayoyafanya ni kwa ajili ya kumfurahisha ili matakwa yao
yakifanikiwa Dk.Salmin Amour aweze kuwapandisha vyeo na
kuwapa marupurupu kwa kazi nzuri waliyoifanya.
Vile vile, ikiwa kweli wanampenda Dk. Salmin Amour kwanza
lazima wawafahamishe wananchi sababu za kutaka aendelee
kwenye awamu ya tatu kwa sababu zifatazo:
(1) Kuwa toka Dr. Salmin alipoanza kuwa Rais wa visiwa hivyo
ameweza kunyanyua hali za wananchi kwa fani mbali mbali.
(2) kuwa Elimu kwa watoto wetu imekuwa bora kuliko hapo kabla
(3) Kuwa hospitali madawa yamejaa na magonjwa mbali mbali
ambayo yaliyokuwa hayawezi kutibika hapo kabla kwa upungufu
wa Madaktri sasa yametoweka.
(4) Kuwa watu hawakamatwi ovyo-ovyo na mtu yeyote yule
anayekamatwa lazima apelekwe mahakamani yafikapo masaa 24.
(5) Kuwa uhalifu wa kuvunjiwa watu majumba na kuporwa vitu vyao
umeshaanza kufifia..
(6) Kuwa wanafunzi wakimaliza skuli makazi yanawangojea.
(6) Kuwa vijana wengi wanabakia nchini badala ya kwenda nchi za
nje kutafuta kazi kwa sababu mahitajiyo yao yameshasawazishwa.
(7) Uhalifi umepunguwa kwa sababu wananchi wanaridhika na hali
ya kimaisha ya kila siku hapo nchini.
Hayo ni machache tu niliyoyaeleza ili iwe kama "chambo" cha
kuwawezesha wananchi kuona kweli Dk. Salmin Amour anastahiki
kuendelea kwa awamu ya tatu pindipo katiba ikibadilishwa kwa
kazi nzuri aliyoifanya.
Pia nimeona nigusie kitu ambacho sifikiri kama kinafaa kuendelea
na jina aliloliacha hayati Mzee Abeid Amani Karume: "Kuwa jela ni
pahala pa chuo cha mafunzo".
Nafikiri wakati umefika kuweza kuita jela kuwa jela siyo chuo cha
mafunzo.
Kwanini nikasema hivyo: Hakuna kati yetu asiyejua mambo
yaliyokuwa yakitokea kwenye hivyo wanavyoviita "vyuo vya
mafunzo", wananchi kutolewa usiku kwenye vyumba vyao na
kwenda kuteswa na kuuwawa.
Wakati wanaoendesha serikali bila hata kuona haya na vibaya
kuendelea kuita sehemu hizo kuwa ni "vyuo vya mafunzo".
Nafikiri itakuwa uzuri kuvita vyuo hivyo sehemu za .
Kwani hakuna asiyejua ndugu zetu 18 mpaka leo wanaendelea
kuteswa kiakili ndani ya hivyo wanavyoviita:" vyuo vya mafunzo".
Hebu tuelezeni kinaga-ubaga hayo masomo munayowapa hao
ndugu zetu 18 toka siku waliokamatwa mpaka hivi leo. Bila ya
shaka watatoka na mashahada ya Phd, BA,nk, nk, nk........
Lazima ndugu zetu munaoendelea kuwatesa,siku yeyote ile
mutakayo amuwa kutaka kuwatowa lazima kwanza muwatake
radhi kwa kitendo mulichowafanyia cha kuwatenga na familia zao
na vile vile muwape fidia kwa muda muliowaweka kwenye hivyo
munavyoviita "vyuo vya mafunzo".
Wakatabahu
Hashil S. Hashil