From: Farouk Abdulla Amour
Subject: DISEMBA 10, SIKU ADHIMU KWA WAZANZIBARI


                      Zanzibar Organization


                  BISMILLAAHI RRAHMAANI RRAHIIM

     "Na shikamaneni kwa Kamba (Dini) ya Mwenyezi Mungu nyote pamoja,
                     wala msifarikiane".



Wazee wetu, Ndugu zetu,

Assalaam Alaaykum, UMOJA NA UHURU


SIKU ADHIMU KWA WAZANZIBARI
Kwa Wazanzibari Disemba 10 ni siku adhimu katika taarikh ya nchi yao, ni 
siku inayoishi katika nyoyo zao kwa fakhari na machungu.  Disemba 10 inaishi 
kwa fakhari nyoyoni mwa Wazanzibari kwa kuwa ndio siku ya Uhuru wa nchi yao. 
Siku ambayo Wazanzibari waliirejeshea nchi yao - Zanzibar - Uhuru wake baada 
ya juhudi zao mbali mbali na kwa kujitolea kwa hali na mali.  Disemba 10 
inaishi katika nyoyo za Wazanzibari kwa machungu na huzni kwa vile Uhuru wa 
Zanzibar na Zanzibar huru haikuishi zaidi ya siku thalathini na tatu, bali 
ilivamiwa na kumezwa na Dodoma chini ya kisingizio cha muungano. Huo ukawa 
ndio mwisho wa Zanzibar na mwanzo wa masaaibu yote ya Zanzibar. Kwa munasaba 
huu adhimu, yaani leo kufika miaka 37 tangu ile Disemba 10, 1963; 
tunamshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu na tunawaombea dua wazee wetu na ndugu 
zetu waliotangulia mbele ya Haki na waliopo ulimwenguni kwa juhudi zao hizo, 
Mwenyezi Mungu awajazi kila la kheri duniani na Akhera - Amin.  Dua zetu 
vilevile ziwafikie wazee na ndugu zetu waliouliwa mashahidi katika ghasia za 
Juni 1961 na katika mavamizi ya Januari, 1964 na mashahidi wetu wote wengine 
wa kabla na wa baada – Mwenyezi Mungu awarehemu na awatie Peponi kwa Rehema 
Zake – Amin.  Kwa munasaba huu, munasaba wa furaha ya wiki chache na 
munasaba wa msiba na masaaibu yanaoendelea mpaka hii leo, Umoja wa 
Wazanzibari – Zanzibar Organization - kwa hishima unaleta mbele yenu humu 
barazani haya yafuatayo ili tushirikiane katika kuzingatia na tufikiri kwa 
pamoja namna ya kutengeneza kwa maslaha ya Zanzibar ya leo na ya kesho.

DOLA HURU YA ZANZIBAR
Kwa Rehma ya Mwenyezi Mungu Mtukufu na juhudi za Wazalendo wa Kizanzibari 
wazee wetu katika uwongozi wa “Umoja wa Wazanzibari” (ZNP/ZPPP), manamo saa 
sita na dakika moja za usiku wa kuamkia taarikhi 10 Disemba 1963; 
waliirejeshea Zanzibar Uhuru wake na kuwa ni Dola Huru Kaamili miongoni mwa 
dola za ulimwengu.  Katika kutekeleza jambo adhimu hilo, bendera nyekundu 
iliteremsh-wa  kutoka kwenye mlingoti wake na Bendera ya Dola Huru ya 
Zanzibar yenye karafuu mbili (zikimaanisha visiwa viwili vya karafuu, Unguja 
na Pemba) ilipandishwa na kupepea katika mlingoti uliokuwepo kwenye ardhi ya 
Zanzibar katika uwanja wa Mivinjeni (Coopers Insititute). Kwa vile Zanzibar 
haikuwa koloni ya Muingereza, basi haikuwepo bendera ya Kiingereza 
kuteremshwa, kwa sababu haikupatapo kupepea juu ya ardhi ya Zanzibar. 
Japokuwa Zanzibar ilitiwa kwa mbinu za Waingereza chini ya himaya ya 
Kiingereza, haikuwa koloni kama vile koloni nyenginezo za Kiingereza.  
Zanzibar haikusita kuwa Dola kwa muda wote iliokuwa chini ya himaya ya 
Muingereza, iliendelea kuwa Dola na kila lake na chake.  Zanzibar imesita 
kuwa Dola baada ya kuvamiwa na kutiwa chini ya makucha ya Dodoma pale 1964.

SHEREHE ZA UHURU
Wananchi wote wakubwa na wadogo, wanaume na wanawake, waliupokea Uhuru wa 
nchi yao kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu na kwa  furaha  na bashasha 
kubwa.  Mji ulikuwa ukin'gara kwa mapambo ya namna mbali mbali. Tamasha hizi 
na zile zilifanywa na wananchi kwa kufurahikia Uhuru wao. Sherehe na mapambo 
hayakuwa Mjini tu, bali mashamba kote. Na huko Pemba nako kulifanywa sherehe 
kama za Unguja, tangu mijini mpaka mashamba. Wazanzibari walijaa tamaa na 
matumainio ya kwamba baada ya juhudi na kazi ngumu ya kuleta Uhuru wao na 
kwa kuondoka mtawala Muingereza sasa wataweza kushirikiana Wazanzibari wote 
bila ya ubaguzi wa aina yoyote ile katika kazi ngumu na ndefu ya kujenga 
nchi yao kwa masalah ya nchi yao. Tamaa na matumainio haya yalitokana na 
imani yao Wazanzibari juu ya uwongozi wa umoja wao - “Umoja wa Wazanzibari” 
- uliojengeka katika misingi ya uadilifu wa haki sawa kwa wote.  Haya, yaani 
uadilifu wa haki sawa kwa wote yalithibitishwa kwa vitendo kama vile 
alivyotueleza Sheikha Ali Muhsin katika kitabu chake: “Conflicts and Harmony 
in Zanzibar”, yeye katueleza haya yafuatayo:

ZNP/ZPPP FOR ALL PEOPLE.
Our very restricted resources compelled us to have our diplomatic offices in 
New York also accredited to Washington, in London accredited to the rest of 
Europe, in Cairo to cover the rest of the Arab world, and in due course 
Indonesia, which was importing the greatest share of our clove production, 
to be the base for the rest of Asia.

While we made certain that the ambassador and the counsellor (his second in 
command) were our political nominees, being supporters of the ZNP/ZPPP 
alliance, we appointed the first secretaries by virtue of merit irrespective 
of their political affiliation. Thus the first secretary to the UN embassy 
happened to be Khamis Hassan Ameir, to the Cairo embassy was Ali Khamis 
(once speaker to the Zanzibar House of Representatives), and the would-be 
first secretary to Indonesia was to be Ali Hassan Mwinyi. (he later became 
President of Tanzania.)  All three were known to us as supporters of the 
ASP.  Professionally they had the capacity to fill the posts, and that was 
all that mattered to us. It was not very easy to convince everybody in our 
party's national executive of the fairness and wisdom of making these 
appointments, but I did manage at last to get unanimous support by reminding 
my colleagues that ours was, from the very beginning, a vanguard party 
working for the whole nation and not for a segment of the population.

Such and other measures began to have a telling effect on the more thinking 
section of the opposition, particularly the younger educated elements 
aspiring for higher things in the future. They were pleasantly surprised to 
find that the ZNP/ZPPP government was being fair and just, and that it 
assessed people according to merit irrespective of their political 
connections. There was even some talk about their joining the ruling 
alliance en masse. This was a threat to the semi-literate leadership of the 
ASP, the newly created Umma party and their common boss across the channel. 
The longer the government stayed in power the more popular it was bound to 
make itself, and the more likely the opposition would be losing support. 
Thus was it imperative that the rebellion had to take place as soon as 
possible. And thus it was that after the general massacre of the thousands 
of the ZNP/ZPPP supporters Karume and his immediate thug supporters began 
murdering one by one the educated elements in the ASP whom they had always 
suspected of considering changing  their allegiance.  Othman Sharif, Kasim 
Hanga, Mdungi Usi, Twala, Jaha Ubwa and many others were liquidated. Dr. 
Kingwaba was disgraced. From being a successful qualified medical officer he 
was put in charge of the post office.  Dr. Ahmed Rashid, a veterinary 
officer made into a Director of Economy, had to flee for his life. He died 
in Britain.
(Conflicts and Harmony in Zanzibar – page 216)

“Umoja Wa Wazanzibari” katika misingi yake kuwa ni Umoja wa Wazanzibari wote 
ulitekeleza mipango yake yote katika misingi hio. Wazanzibari walitambua 
vyema kuwa baada ya hivi kupatikana Uhuru kulikuwa na kazi kuu mbele yao, 
yaani kujenga nchi ni kazi ndefu na ngumu sawa au zaidi kuliko ile ya kuleta 
Uhuru.  Juu ya hivyo, walikuwa tayari kubeba jukumu hilo kwa azma na shajaa 
kwa sababu imani yao ni kwamba utumishi wa nchi ni wajibu wa kila mwananchi 
na ni wenye kuhisabiwa na kulipwa mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

ZANZIBAR INAJIUNGA NA UMOJA WA MATAIFA
Baada ya kupata Uhuru wake Zanzibar, taarikh 14 Disemba, 1963 ilijiunga na 
Jumuia ya Umoja wa Mataifa (UNO) ikiwa ni mwanachama kamili wa Jumuiya hio 
ya kilimwengu. Kwa munasaba huu nina inukulu hapa (tena) khutuba ya Waziri 
Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Muhammad Shamte katika Umoja wa Mataifa (UNO) 
taarikhi 16 Desemba, 1964 ikikaribishwa Zanzibar kuwa ni mwanachama wa 
Jumuia hii  muhimu ya kilimwengu.

A REMINDER SPEECH
Prime Minister Muhammed Shamte Hamad (as Head of Government of the 
independent and Sovereign State of Zanzibar) delivered the following 
historic speech on the historic day of 16th December, 1963 to the General 
Assembly of the United Nations Organization in New York.

Mr. President!
It is a very great honour and a very great pleasure for me to be here as 
Zanzibar's representative at the moment when Zanzibar's application to join 
the United Nations Organization has been accepted by the General Assembly.  
Zanzibar's entry to this great Organization is to my mind of special 
significance, and this is that there is no country so small and so modest in 
its means that it cannot be represented here in equal terms with the great 
nations of the world.  There are some people who consider this scheme of 
things to be wrong.  But I consider it to be a source of strength to this 
Organization, and that one that will inspire Zanzibar to use its privileges 
with a sense of responsibility and dedication to the ideals which prompted 
the establishment of the United Nations.

To our many friends throughout the world who have done so much in supporting 
our struggle towards national liberation, to the Decolonization Committee 
which has contributed so much in speeding up our march to Independence, and 
to this august Organization of the United Nations to which we owe so much, I 
would like to convey my country's deep gratitude.  To them we continue to 
look for aid and support in the upliftment of our people so that we may also 
be able to contribute our humble share towards the solution of the world's 
problems. To the distinguished delegates in the Security Council and in this 
General Assembly who paid tributes to the struggle and achievements of my 
country I would like to convey the sincere gratitude of my delegation.  To 
all those who have sponsored our application, and to all the distinguished 
delegates who have unanimously voted us into membership of the United 
Nations, I say: Thank you.

Mr. President.  Political problems tend to hit the world headlines, but it 
is not generally known, for instance, that malaria which a few years ago 
used to cause as much havoc as any war, is now almost wiped out from 
Zanzibar, as a result of an intensive joint effort on the part of WHO, 
UNICIEF and the Government and people of Zanzibar.  It is also not known 
that quietly but determinantly we are trying with the aid of the ILO and FAO 
to do away with the curse of under-employment.  There are many other ways in 
which individual countries and international organizations have been 
co-operating with us in solving our problems.  We are grateful to them all.

Now that the energies of our people are unleashed by the restoration of our 
national pride and sovereignty we can look forward with confidence to 
greater and more comprehensive assistance from every quarter.  Zanzibar is 
one of the smallest nations in terms of population and size to be accepted 
for membership.  This in itself entails sacrifices for Zanzibar, sacrifices 
which are of little significance to nations of great wealth, but are of very 
great concern to us of slender means.  These sacrifices we are very glad to 
make.  If we are not rich in numbers, in territory, in material wealth we do 
not count ourselves poor in values of life which are so inestimably more 
important; and it is because of this that we feel we can contribute, even if 
only modestly, in the affairs of this Assembly.

We have a long and honourable history and civilization behind us.  Like so 
many of the great peoples of the world our roots are sprung from many 
different sources, from Africa primarily, but also from Arabia, from the 
civilization of Asia, Persia, from India and from many others.  The 
Europeans in their great voyages of exploration found succour and sustenance 
on our shores.  And men of many races found rest and stability in our 
islands from where to organize the exploration and development of Central 
and Eastern Africa It is due to these roots established over centuries, the 
mixing of so many cultures, that make us proud of our reputation for 
moderation and friendliness.  While in the modern world we do not intend 
looking back to our past, it is this tradition on which we intend to build 
our future.

Zanzibar is a constitutional monarchy founded on liberal and democratic 
traditions, governed by a Prime Minister and a Cabinet of elected Ministers, 
with collective responsibility and answerable to a National Assembly elected 
on the basis of universal adult suffrage.  The Fundamental Human Rights to 
personal liberty and protection against discrimination are entrenched in 
Zanzibar's Constitution.  Our overall aims are peace and progress at home 
and abroad.  The chief object must be to help create a political atmosphere 
in the world in which man's real enemies of hunger, ignorance and disease 
can receive full attention so that resources and time are not wasted on 
fruitless matters of dissension.  Zanzibar's general policy is one of 
benevolent and positive neutrality without discrimination against any 
country on grounds of race, creed, culture or ideology.  It supports all 
measures of peace in the world on the basis of international cooperation. On 
the achievement of its independence Zanzibar has freely elected to remain a 
Member of the Commonwealth of Nations, and it is fitting and pleasurable to 
pay tribute to the continuing harmonious relations which have obtained 
between Zanzibar and the United Kingdom.  We believe in the Commonwealth as 
a large number of equal and sovereign states of many peoples and cultures 
who have voluntarily and democratically joined together and are dedicated to 
the furtherance of peace, co-operation and prosperity throughout the world.

It is the object of Zanzibar to strengthen the many ties it possesses with 
both Africa and the East.  To this end we subscribe to the principles of the 
Bandung Declaration of 1955 and of the Charter of the Organization of 
African Unity framed at Addis Ababa this year.  Zanzibar has particularly 
close relationship with the other territories of East Africa, and it is our 
intention to continue this in friendship and co-operation, whether inside or 
out of a form of an East African Federation.  In this respect I am 
particularly glad that Kenya with which Zanzibar has so many close 
connections is being welcomed into this Assembly at the same time.  At this 
proud moment in our history I may be permitted to quote Shakespeare and say: 
"We are two lions littered in one day."

Sir, In submitting the application for membership for Zanzibar I have made a 
solemn declaration in common with that made by other nations represented 
here today that on behalf of my government I have accepted the obligations 
contained in the Charter of the United Nations, and have undertaken to 
fulfil them.  This solemn declaration is a very real one for me, and I pray 
that this indeed will be so, and that Zanzibar in future will honour it to 
the full.  Thank you, Sir.

MAVAMIZI YA JANUARI 12, 1964
Ole wetu!  vitumishi vilikuwa vimeshawekwa tayari na mabwana zao kuufisidi 
na kuuvuruga Uhuru, bali kuivuruga Nchi na  wananchi wake.  Sherehe 
hazikuwahi kumalizika, wala majasho hayakuwahi kukauka mwilini kutokana na 
juhudi na mbio za kugombea Uhuru wetu, bali ghafla tulijishitukia katika 
msiba, tushavamiwa.  Na huo ulikuwa ndio kuanzia kwa maafa ya Zanzibar na 
kupotea kwa kila kheri yake na kumezwa Dola ya Zanzibar na kutiwa chini ya 
makucha ya Dodoma kwa kisingizio cha muungano.

Mafisadi wachache kwa ajili ya maslahi  ya nafsi zao hawakutahayari wala 
hawakuona vibaya hata kidogo kuchan-ganyika  na wageni waliokuwepo ndani ya 
nchi na walioletwa kutoka nchi za jirani kwa makusudio khasa ya kuivamia 
Zanzibar na kuiondoa Serikali ya wanan-chi  na kuimeza Dola ya Zanzibar. 
Wananchi mafisadi hao walikubali kuongozwa na wageni, John Okello aliyetoka 
kwao Uganda, Injin aliyetoka kwao Kenya na Mfaranyaki aliyetoka kwao 
Tanganyika,  kuivamia nchi yao katika siku  wa manane wa kuamkia taarikh 12 
Januari 1964. Wananchi, mafisadi kwa sababu ya maslahi ya nafsi zao 
hawakuhisi  uchungu wala fedheha kuipoteza nchi yao, wala kuzipoteza roho za 
wazee wao, za ndugu zao na za marafiki zao. Kwa mujibu wa kitabu cha huyo 
aliyejipa ujamadari wa hayo 'mavamizi' ya Januari 12, 1964, John Okello, 
amesema kuwa watu waliokufa (waliouliwa) katika 'mavamizi' hayo ni 13,000.  
Hii ni idadi ndogo kabisa aliyopenda kuitaja yeye.

Ukatili, ushenzi na unyama uliofanywa katika visiwa hivi vilivyokuwa na 
ustaarabu wa kupigiwa mfano, hauwezi hata kuhadithika. Wengi waliokuwa 
wanaijua Zanzibar, waliona taabu kuyaamini waliyokuwa wameyasikia yametokea 
Zanzibar kutokana na hayo yenye kuitwa 'mapinduzi'.  Ilifika hadi, siku hiyo 
ya 'mavamizi' majahil na makatili hao ku-wanajisi maiti wa kike. Kitendo 
hicho hakijapa-tapo  kufanyika  katika nchi nyingi ulimwenguni zenye 
ubinaadamu na ustaarabu wake.

MWALIMU NA MAVAMIZI YA ZANZIBAR
Sote tunakumbuka uzuri maneno ya Mwalimu aliposema, “Lau kuwa nnaweza basi 
ningali viburura Visiwa hivi (Zanzibar) hadi katikati ya Bahari ya Hindi”.  
Na hivyo ndivyo alivyokuwa akifanya Nyerere mpaka kuondoka kwake ulimwenguni 
na ndivyo wanavyofanya warithi wake hadi hii leo, wamo kuviburura Visiwa 
vyetu kuelekea baharini. Tafauti iliyopo baina ya jana na  leo ni kuwa hii  
leo vuta-ni-kuvute baina ya Dodoma na Wazalendo wa Kizanzibari imezidi kuwa 
kubwa kwa vile kila siku upande wa  wananchi  unazidi Umma  na unazidi 
nguvu.  Umma unazidi kufahamu madhila ya kutawaliwa na haja ya kurejesha 
Dola yao Huru ya Zanzibar ili warejeshe ubinadamu wao na waweze kuishi 
kibinadamu.

KUMEZWA DOLA YA ZANZIBAR
Sote tunafahamu ya kwamba mara baada ya mavamizi ya Januari 1964, mwaka huo 
huo; mwezi wa Aprili Zanzibar ilitiwa chini ya makucha ya Dodoma kwa 
kisingizio cha muungano. Kutokana na “Articles of Unions” Zanzibar ilipoteza 
Dola yake na kuwa ni koloni la Tanganyika.  Mengi yamesemwa juu ya suala 
hili, ya hivi karibuni ni haya waliosema wao wenyewe, katika kitabu chake 
“The Political Plight of Zanzibar”, Profesa Maliyamkono katika ukurasa wa 
198-199 ametueleza haya kukhusu huu unaoitwa muungano:

“Defining Union Matters
One of the thorniest problems facing the Union has been that of deciding on 
the formula for the relative contribution of each part of the Union to the 
fiscal requirements of the Union.  This requires first a decision or what 
government activities should constitute Union matters. Constitutionally, the 
Union matters have their history in the “Articles of the Union”, signed by 
the two founders of the Union, Mwalimu Julius K. Nyerere, on behalf of 
Tanganyika, and Sheikh Abeid Karume, on behalf of Zanzibar.

The Interim Constitution based on the Articles of the Union, stated that the 
issues for which the Union Government and Union Parliament had direct 
responsibility were these:

1. The Constitutions and Government of the United Republic
2. External Affairs
3. Defence
4. Emergency Powers
5. Citizenship
6. Immigration
7. External Trade and External Loans
8. The Public Service of the United Republic
9. Income and Corporate Tax, Customs and Excise Tax
10. Harbous, Civil Aviation Post, and telegraphs

It is however, debatable whether all the above 10 areas are exclusively 
Union matters as the Interim Constitution may have intended them to be. 
Obvious queries arise with regard to 7 & 8, for example.  With regard to No. 
7, Zanzibar runs its own external trade and even keeps its own statistic on 
foreign trade and payments. As for No. 8 the implication is that there is a 
Union Service Commission.
There is none.

The list of Union “matters” was increased to 21 when the Constitution of the 
United Republic was published in 1997.  These were:

11. All Banking and Currency Matters
12. Industrial Licences and Statistics
13. Higher Education
14. Petroleum Natural Resources
15. National Examination Council
16. Air Transport and Communication
17. Research
18. Meteorology
19. Statistics
20. United Republic Court of Appeal
21. Registration of Political parties

Again it is doubtful that all these additional activities are exclusively on 
effectively Union Matters

The Shellukindo Committee (see below) expanded the scope of the Union based 
on the argument that most ministries in SMT have some Union element.  Thus 
the Presidency is to a certain extent a union matter.  Every ministry in the 
SMT which deals with international agencies on behalf of the entire United 
Republic is involved in a “Union” activity.  This is the widest definition 
of Union matters and the definition in the Interim Government is the 
narrowest.”

Ndugu zangu, huu ndio muungano; muungano ambao tangu ulipoundwa ulikwisha 
ipoteza Dola ya Zanzibar kwa kunyang’anywa Zanzibar mambo 10 ambayo ndio uti 
wa mgongo wa Dola.  Baadae polepole ndio 11 mengine kuongezwa na hapa 
kuimaliza Zanzibar. Yote haya ni kizungumkuti, hapana lenye kufahamika; ni 
kuzongwazongwa tu,  lakini haya maneno: “Thus the Presidency is to a certain 
extent a union matter”, ndio zaidi hayafahamiki.  Jee Raisi wa Zanzibar ana 
uwezo gani? Kwa kumaliza muandishi ametwambia kuwa: “This is the widest 
definition of Union matters and the definition in the Interim Government is 
the narrowest”.  Kweli ilioje! Kweli ikidhihiri uwongo hujitenga.

Wazee wetu, ndugu zetu, Wazanzibari huu ndio “muungano” na hivi ndivyo 
ilivyofikishwa Zanzibar ndani ya huu “muungano”.

Matumainio yetu sote ni kwamba sisi ni watu wazima na wenye fahamu kamili, 
sio watoto wadogo wala sio tusiofahamu.  Mwenye macho haambiwi tizama.  Nini 
la kutenda hili ndio suala muhimu, lakini la kutenda ni lazima Wazanzibari 
waamue na kwa haraka kwani kila tukichelewa ndio khatari inazidi.   “The 
list of Union “matters” was increased to 21 [when the Constitution of the 
United Republic was published] in 1977.”  Hapa haioneshi kuwa hii 
constitution inayosemwa kuwa ilizungumzwa na kukubaliwa na kila upande - 
Zanzibar na Tanganyika - kisha ndio ikawa “published”.  Msiba ni kwamba 
inawezekana wakati wowote ule hii constitution ikawa “published” na 
kuongezwa orodha nyengine, kama kiko bado ambacho hakijachukuliwa na kutiwa 
ndani ya huyu jini anaeitwa “Union matters”.

DHULMA NI MOTO USIOKUWA NA BWANA
Kutokana na fisadi na fitina zilizokuwa zikiongozwa na Nyerere na kusaidiwa 
na mabwana zake pamoja na vibaraka vyao, Zanzibar ilivamiwa na kutiwa chini 
ya utawala wa Dodoma kwa kisingizio cha muungano.  Yote haya ni kuendeleza 
vita vya msalaba dhidi ya Waislamu.  Walimwengu mbali mbali kwa kusikiliza 
fitina hizo - ambazo zilipandikizwa kuwa ati iliopinduliwa Zanzibar ni 
serikali ya Kisultani na Kiarabu - walisherehekea maovu yote yale 
yaliotendewa Zanzibar.  Wengi wa walimwengu walikuja Zanzibar kusherehekea 
mauaji, kunajisiwa binadamu – wake kwa waume, wakubwa kwa wadogo; 
kunyang’anywa watu haki zao, tujazwa magerezani mamia ya binadamu bila ya 
kosa na bila ya kupelekwa mahakamani, kuwabidi mamia ya binadamu kuihama 
nchi yao bila ya kujuwa wanakimbilia wapi.  Walimwengu walisherehekea na 
kuyakiri maovu hayo, walimwengu hao wakiwemo Waislamu walikiri kutendewa 
binadamu dhulma. Dhulma hii walifanyiwa Wazanzibari, lakini walisahau kuwa 
dhulma ni moto, moto hauna mipaka wala hauna bwana. Moto huu wa dhulma 
ulienea ghafla Afrika nzima, kuanzia Afrika Mashariki na kwengineko. 
Serikali kadhaa wa kadhaa zilipinduliwa na watu kupata kila maafa, wengi 
iliwabidi wazihame nchi zao ili kukimbia maovu waliokuwa wakitendeana 
wenyewe kwa wenyewe.  Mnyonge kudhiliwa ilikuwa ndio mtindo wa kila siku.  
Haya yote ni kwa sababu ilipotokea dhulma Zanzibar hapana alieinua sauti 
yake kuiteta, kinyume chake, wengi waliikiri na kuisherehekea, kwa sababu 
Nyerere kawaambia kuwa waliofanyiwa hivyo ni kina sultani – kwahivyo wanafaa 
kudhulumiwa.  Walisahau kuwa dhulma ni moto, hauna mipaka wala hauna bwana.

HATUTENGENEKEWI  MPAKA TUONDOE  DHULMA
Wazanzibari tusitaraji kupata Nusra ya Mwenyezi Mungu mpaka kwanza tutake 
toba ya kweli, hapo tena ndio tuombe Nusra ya Mwenyezi Mungu ambayo ndio 
pekee itakayo tuvua na maafa na balaa hii tunayoishi nayo tangu pale 
tulipoingia katika dhulma.  Toba ya kweli ina shuruti zake,  miongoni mwa 
shuruti hizo ni kujuta kwa tuliotenda na kuazimia tusirejee tena kutenda 
maovu hayo.  Vilevile shuruti zake ni kutenda mema kwa kuondoa dhulma na 
kuleta haki na kumpa kila mwenye haki yake haki yake.  Haiwezekani kujenga 
haki na uadilifu juu ya dhulma, ni lazima kwanza tuondoe dhulma ndio tuweze 
kujenga haki na uadilifu.  Huwezi kupanda mmea ndani ya biwi la moto.

TUME YA KUCHUNGUA DHULMA
Kwa makusudio ya kutengeneza na kutafuta Nusra ya Mwenyezi Mungu kwa kuondoa 
dhulma na kujenga haki na uadilifu tunamuomba Bwana Aman ateue tume maalumu 
ichungue juu ya dhulma zote tulizotendeana na kupangwa njia ya kuziondoa 
dhulma hizo na kujenga haki na uadilifu badala yake.  Kitendo hichi ni cha 
dharura ili tuweze kupata Nusra ya Mwenyezi Mungu na tuweze kutarajia 
kuokoka kutokana na haya maafa tunayoishi nayo tangu pale tulipojitia katika 
dhulma kwa mikono yetu.

SERIKALI  YA UMMA NDIO HAJA YA UMMA
Matokeo ya uchaguzi wote uliofanywa Zanzibar tangu wa 1961 na mpaka wa 1963, 
wa 1995 na huu wa leo 2000;  yote inaonesha na kuthibitisha haja ya Umma wa 
Zanzibar kuwa haja yao ni “Serikali ya Umma”. Umma wa Zanzibar haukubali 
kugawika mafungu mafungu, hata kama vitaletwa vyama zaidi ya ishirini.  Umma 
wa Zanzibar uamuzi wao ndio ule ule, tangu mababu, mababa na hata watoto, na 
ndivyo itakavyokuwa hata kwa wajukuu na vilembwe.  Umma wa Zanzibar ushaamua 
na maamuzi yao ndio ya mwisho, haja ya Umma wa Zanzibar ni Serikali ya Umma. 
Wazanzibari hawataki kuzidi kufarikishwa kwa kugawiwa vifungu vifungu. 
Waliokuwa ZNP/ZPPP ndio weshakuwa na waliokuwa ASP ndio weshakuwa. Ni wajibu 
wa ndugu zetu walioko katika uwongozi waikubali hali ilivyo na kwa ilivyo 
ndivyo twende, kutaka la muhali ni muhali; kutaka Wazanzibari wabadilike ni 
muhali na kwenda kinyume na matakwa ya Umma ni kutaka muhali. Umoja wa 
Wazanzibari muda wote huo ulikuwa daima unalingania kuundwa Serikali ya 
Umma, kwa vile kufahamu umuhimu wake na kwa kutambuwa matakwa ya 
Wazanzibari. Umoja wa Wazanzibari uliendelea na unaendelea kulingania 
Serikali ya Umma mpaka hii leo.

SERIKALI IMEFANYA MWANZO MWEMA
Alhamdulillah serikali chini ya uwongozi wa ndugu yetu Bwana Aman Abeid Aman 
imeanza kwa kuleta ishara njema za kutaka kuleta umoja wa Wazanzibai kwa 
hivi kuchaguwa Baraza la Mawaziri ambalo linamathili zaidi uwananchi.  Hii 
ni khatuwa njema ambayo ni busara kuipa mwega zaidi na kuiombea kheri na 
mafanikio.  Lakini basi, itakuwa ni busara na kheri zaidi iwapo Sheikh Aman 
atachukuwa khatuwa zaidi  na kuwataka ndugu zetu CUF kuingia katika serikali 
kwa kuundwa Serikali ya Umma.  Hapana shaka kuwa na ndugu zetu CUF kwa 
maslaha ya nchi yetu wataipokea khatuwa hio kwa moyo mkunjufu na 
kushirikiana na kufungua ukurasa mpya. Kama inavyoaminiwa na wengi kuwa CCM 
na CUF wanao kiasi ya 90% ya Umma wa Zanzibar na kiasi ya 10% ndio sehemu ya 
Umma ambo kwa ilivyo ni kuwa wao hawana chama maalumu. Wote hawa ni wananchi 
na wana Haki na Wajibu sawa ambao ni lazima kutekelezwa kwa kushirikishwa 
katika serikali yao, hivyo ndivyo itakavyofanya hio “Serikali ya Umma”,  
serikali ya wananchi wote.

MASHAURI JUU YA HIO SERIKALI YA UMMA
Kukhusu hio “Serikali ya Umma” tunapenda kutoa raia kuwa iwe  ya muda wa 
miaka sita badala ya miaka mitano, na kila upande upate fursa ya kuwa katika 
uwongozi wa Serikali hio kwa kipindi cha miaka mitatu.  Hivi kwa maana miaka 
mitatu ya mwanzo kwa mfano CCM ndio watakaochagua Rais na CUF watachagua 
Waziri Mkuu.  Na baada ya miaka mitatu watabadilisha,  CUF watachagua Rais 
na CCM watachagua Waziri Mkuu.  Vilevile, ikiwa hio Serikali ya Umma ina 
mawaziri 14, basi sita iwe kutoka katika CCM na sita kutoka katika CUF na 
wawili kutoka katika huo Umma wa 10%. Hali hii itawafanya wananchi wote 
kupata kushirikishwa katika serikali ya nchi yao bila ya ubaguzi kutokana na 
fikra za kisiasa au ubaguzi wowote ule.

KAMATI ZA UTENDAJI
Badala ya Waziri, ni kuundwa Kamati ya Utendaji, kamati hizi zitakuwa badala 
ya Waziri;  kwa mfano badala ya Waziri wa Fedha itakuwa ni Kamati ya Fedha.  
Kwa mfano kila Kamati itakuwa na wawakilishi watano, wawili kutoka katika 
CCM na watatu kutoka katika CUF na Kamati nyengine itakuwa na Wawakilishi 
watatu wa CCM na wawili wa CUF, na kadhaalika.  Wawakilishi watano hawa 
wanne watakuwa ni wanachama wa hio kamati yao na mmoja wao kati ya hao wanne 
atakuwa ni mwanachama na Katibu wa Kamati yao na watano wao ndie ataekuwa 
Mwenyekiti wa Kamati.  Nyadhifa hizi zitakuwa kwa kubadilishana kwa baada ya 
kila muda.  Mpango huu licha ya kuwa utawapa Wawakilishi nyenzo ya 
kuthibitisha uwezo wao katika kutekeleza dhamana walizotwika na Umma 
waliowachaguwa, Umma unaotarajia upate utumishi wa Wawakilishi wao, bali 
zaidi utaondoa uwezekano wa ubadhirifu wa mali ya Umma na utumiaji muovu wa 
wadhifa na uzorotaji wa utendaji na utekelezaji.  Zaidi ya haya, mpango huu 
utaleta utaratibu wa kuwepo “collective responsibility and accountability” 
juu ya wote watakaoshiriki katika utumishi wa serikali.  Ikiwa ni sifa ni 
sifa ya wote, na ikiwa upungufu ni wote ndio wenye kuhisabiwa kwa upungufu 
huo.

SERIKALI YA UMMA HAIMUONDOI WA ZAMANI
Kwa maumbile yetu, na kwa ilivyofanywa;  kufika katika madaraka imekuwa ni 
njia ya kipato na njia ya kujijengea fakhari na kiburi.  Kutokana na hali 
hii, wengi wetu tunataka “kufa kupona” lakini nifike katika utawala (na 
nisitoke katika utawala) ili niweze kupata chochote na niweze kuwa bwana 
mkubwa, niweze kutenda ninavyopenda bila suala wala jawabu.  Niweze kuchuma 
(kwa njia ya haramu) kwa upesi kama nitakavyo weza kabla ya kuondoka kwenye 
utawala. Nihakikishe kuwa sitoki katika utamu na raha hizi. Hali hii haiwezi 
kufutika nyoyoni mwetu leo au kesho, itachukuwa muda; muda ambao utalazimu 
uwe na mfunzo ya kuendelea na kudumu juu ya “UWONGOZI NA DHAMANA ZAKE”.  
Inahitaji tumjuwe na tumche Mwenyezi Mungu katika dhamana ya uwongozi, hapo 
ndipo tutakapoweza kupata waongozi wa kheri, waongozi waaminifu.  Safari ni 
ndefu kufikia huko, lakini penye nia pana njia – Inshallah tutafika – Amin.  
Kwa hivi sasa ni busara kuwa bwana wa zamani awepo asipigwe pute mkate wake 
na bwana wa leo nae asinyimwe fursa ya mkate – madhali Umma umewachaguwa.  
Ilivyo ni kwamba Serikali ya Umma haimtoi wa jana wala hamzuilii wa leo 
kuingia katika utawala.  Sote tutakuwemo, kila mmoja atapata sehemu yake.  
(kila mmoja atabeba mzigo wake – mzigo wa dhamana za uwongozi – hesabu 
Kesho).  Tunamuomba Mwenyezi Mungu  Mtukufu atusaidie tuweze kujisaidia 
katika utekelezaji wa  dhamana za uwongozi – Amin.


KUTENGENEZWA KATIBA
Kwa kujikinga na uwovu wa uwezo (power) ni muhimu ziwepo kanuni madhaubuti 
za kuwahifadhi na kuwahisabu mabwana wanaokuwa katika madaraka. Tusisahau 
kuwa sisi ni binadamu na binadamu ni mwingi na mwepesi wa kughurika na 
tusisahau kuwa:  “power corrupts and obsulute power corrupts obsulutely”. 
Kutokana na hali hii ni dharura tuwe na Katiba ambayo ina hifadhi haki za 
mwongozwa na haki za mwongozi.  Katiba ambayo itabainisha na kuhifadhi “Haki 
na Wajibu” wa kila mmoja wetu kwa uadilifu kabisa. Katiba ambayo haitaruhusu 
yeyote yule kuwa juu ya kanuni, kanuni ndio itakayokuwa juu ya kila kitu. 
Katiba ambayo kwa haraka kabisa itazifuta zile Sharia Ovu Arubaini zilizo 
orodhishwa katika tume ya Jaji Nyalali na kuhakisha kuwa hazitaletwa tena 
katika kanuni za nchi kanuni kama hizo au za mfano wake.

Kwa kumaliza, tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu ajaalie hii dhamiri na nia 
ya kuundwa “Serikali ya Umma” ithibiti na itekelezwe kwa salama na amani kwa 
manufaa ya vizazi vyetu na jamii ya binadamu – Amin, Amin.


WA BILLAH TAWFIQ



Umoja Wa Wazanzibari
Disemba 09, 2000







To subscribe to ZANZINET go to http://www.zanzinet.org/register.html
To unsubscribe send "unsubscribe" command to: zanzinet-request@zanzinet.org
For the list of ZANZINET members send "who" command to above address


Visit ZANZINET Web Site