Shilingi In-geleka!
27 Feb 2000
Wenzangu nawakumbusha, kuhusu hii shilingi,
Jana neipata machumini, kazini nlikokuwa,
Haiweka nfukoni, nkenda zangu nyumbani,
Shilingi in-geleka, chakukila sitimizi.
Kutwa jana nehangaika, majasho yakinitoka,
Roho ilinikauka, shilingi ndo haipata,
Nikaingia nyumbani, mchagoni haiweka,
Shilingi in-geleka, chakukila stimizi.
Nemka unjuye, nje nikajiendea,
Nikafanya la kufanya, kisha harudia ndani,
Nkenda mchagoni, kuifuata shilingi,
Shilingi in-geleka, chakukila sitimizi.
Hamwendea baba yangu, kumpa hii habari,
Akasema kanechoka, na shilingi isodumu,
Akanipa yake rai, niache kuitegemea,
Shilingi in-geleka, chakukila sitimizi.
Kasema niache kazi, nfanye yangu mwenyewe,
Itakuwa na thamani, na hadhi ya kusifika,
Itaimarisha nyumba, mashaka konokea,
Shilingi in-geleka, chakukila sitimizi.
Mie hii shilingi, yanichosha maboye,
Bora nimsikilize baba, kazi nianzishe,
Ntapata yangu shilingi, kamwe haitageleka,
Shilingi in-geleka, chakukila sitimizi.
Mtungaji:
Mohammed al-Nabhany
B.A - E.L
Toronto