.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Kioo

 

 

 

 

 

 

Related links

Kioo!

Date:  22 Mar 2001

Kioo kinapumbaza, wangapi wapumbazika
Wengine kinawalaza, namajoho kuwavika
Sifa yake miujiza, viumbe waathirika
Kuwa wewe kwenye kiza, kauli umeumbika
Wengine hukiapiza, miko machozi kutoka
Chatowa jina aziza, wendako unasifika
Simdogo siajuza, wote kwake malaika
Chakupamba chakuliza, wanguruma mwananyika
Wajinata chakucheza, kumbe unamungunyika
Kioo kukichunguza, wateleza wachujuka

 

Hashil

Kioo!

Date:  22 Mar 2001

  1. Kama ukaninunua, Hajazo hakufanyia
    Penye kovu hakwambia, Tena ukazingatia
    Jipulo ukalivizia, Na uso ukajikwabua
    Kioo nakukosa nini?, Hebu nifafanulia
  2. Sinalo lakuzidisha, Ulivyo ndivyo najua
    Tena hakukumbusha, Usowo matongo sikia
    Tena hakuamsha, Upendeze kwa yako njia
    Kioo sinitie makosani, Bwana nakuangukia
  3. Hivyo upewe kisu, Ukamchinje ngamia!
    Halafu useme usu, Bora nimchinje Rabia
    Hilo sikosa la kisu, La wewe ulivyoamua
    Kioo yanihusu nini?, Kosa ni lako sikia!
  4. Amkeni waungwana, Muitizame dunia
    Makosa kutupiana, Na lawama kila njia
    Si mtu huwa avuna, Alichopanda, sheria?
    Kwa makosa siyaoni, Kumbuka ulivyonitumia.

 

Ali Rashid Salim

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet