|
|
Nasaha!
16 Dec 2001
- Laana, kuteremkia watu, kwanza awali, hunyosheana vidole
Bayana, wakaondosha na utu, hata wawili, hupigiana kelele
Uwana, kwa panga na mirututu, si mbali, huyu kuuwa wa yule
Maana, dhaifu imani zetu, na dalili, kwa bayana twaziona
Ibrahim Noor
Nasaha!
17 Dec 2001
-
Laana, ada ikifurutu, wenye akili, hugeuka wapole
Hiyana, ya mtu na mtu, huhasiri mali, tele wa tele
Amana, za wingi wa vitu, vya asili, na vya kale
Maana, uchafu wa roho zetu, na dalili, kwa bayana
twaziona.
- Laana, viamboni na misitu, hukalili, ukubwa wa makole
Hakuna, cha kujaa upatu, cha kumtosha fahali, wana na
wavyele
Hasana, hairudi katu, na kusema kweli, haitarudi
milele
Maana, ufisadi wa nyoyo zetu, na dalili, kwa bayana
twaziona.
- Laana, yazidisha papatu, ikaondoa adili, pole pole
Hapana, anayethubutu, kujifanya dalali, akatoka mbele
Amina, ewe mola wetu, twaomba jamali, na utuongole
Maana, hafifu ibada zetu, na dalili, kwa bayana twaziona.
Kassim O. Ali
|