|
|
Tamu ya Wali!
18 July 2001
- Si lazima kwa mchuzi, ladha wali kuibaini
Pilau kwa nyama mbuzi, inapikwa majumbani
Na wapishi wamaizi, huipamba biriyani
Tukawa hatujuwani, tonge vinywani hujazwa
- Kuna na wali wa kamba, ladhaye hujaijuwa
Na kwa cha bwana-kilemba, mchicha au mayugwa
Sifaze nitaziwamba, wajuwe wasozijuwa
Sufuria wakanguwa, Mkonowo wauramba
- Mkonowo wauramba, kipikwa ukapikika
Kitumbo kikavimba, lepelepe hukushika
Huchelei na kuyumba, hadhara waaibika
Bara-Hindi hadi Pemba, Nyali hujazila nyali
Ibrahim Noor
|