.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Upo Upo Hapo?

 

 

 

 

 

 

Related links

Upo Upo Hapo?

Date:  5 April 2001

  1. Nasikia kuna kitu, jina lake umekwisha
    Nahalafu kuna mwitu, jina lake unataisha
    Nenda zako huna kitu, machachari yasokwisha
    Nipishe mzee chatu, kazi yako kuulisha.
  2. Mama mwanawe ataka, maziwa kumnyonyesha
    Alia mithili paka, namachozi yanamwisha
    Vurumai na mashaka, ndiyo yanomuyayusha
    Kijiwe kinampaka, tumechoka kukodisha.
  3. Siti rejea nyumbani, nyimbo zako zasifika
    Zikitutia imani, kila kipembe zafika
    Umebakia moyoni, kishada kilotoweka
    Lakufanya liko pwani, kuyoyoma kujizika.
  4. Penye wengi panamengi, tusijifanye vizoro
    Porini kuna shilingi, na pia makorokoro
    Posimo mimi gingingi, mambo hayo ni uharo
    Paparika hutupingi, ni njia ya che.kovaro.

 

Hashil

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet