.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Mlolala Amkeni

 

Related links

 

Mlolala Amkeni!


Date: 26 Aug 2002

  1. Ndugu zangu amkeni, nje kushapambazuka
    Haraka natutokeni, jogoo limeshawika
    Tusisimame twendeni, tena tufanye haraka
    Zanzibar imipangoni, wabara kujaiteka
    Tuwe macho sidhihaka

  2. Mbinu zinajibaini, kila kukicha ningeni
    Nasi tumo hatarini, kama hatuko makini
    Hawa sio majununi, wanayofanya yakini
    Nia ni kutuhaini, watuzamishe majini
    Wenzangu tahadharini

  3. Tulikuwa tuna vyetu, tajiri wa kila hali
    Mahasidi hawa watu, wevi wa zetu mali
    Hawakubakisha kitu, ila kimoja viwili
    Mikubwa hii michatu, watumeza kweli kweli
    Tuweke yetu akili

  4. Bado wamo mawindoni, kutaka kutumaliza
    Waliyo madarakani, wambele kushindikiza
    Wajifanya hamkwani, wamo kutuangamiza
    Inatilisha huzuni, wenzetu wanatuuza
    Haya siyakupuuza

  5. Tusimameni kidete, tuzivunje nguvu zao
    Kwa umoja tuwe sote, tuwatowe wende kwao
    Mungu katuumba wote, dola kila watu lao
    Kutembea ni popote, sio kuchukuwa chao
    Bora kutengana nao

 

Maher Fundi.

 

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet