.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Ntampiga kwa Mbali

 

Related links

Ntampiga kwa mbali

Date: 16 May, 2003

  1. Fundi hatafuti mbili, moja ya ndani yatosha
    Wala sitangi kwa hili, cha mbele huporomosha
    Kama haya hukubali, kiweke takuonesha
    Ntakipiga kwa mbali, kama nnakiamsha


  2. Iwe ndogo ya sindano, tundu ya kiasi hicho
    Umbali uso mfano, kipande ukijuwacho
    Sitolitafuna jino, wala kupepesa jicho
    Ntakitowa kibano, kiruke kisiwe nacho


  3. Sisaki kwenye vichaka, kwa mshare na upinde
    Langu ni pori la nyika, mkuki huwa upande
    Nikirusha nihakika, wateleza na umande
    Ukapiga kwa haraka, akafa na usigande


  4. Sasa nnakuwalika, twende sote usasini
    Shuruti hutoshituka, kuyaogopa majani
    Au vinopukutika, nakuanguka mitini
    Tukamkamate nyoka, tumtiye guniani


  5. Yako ya mbali ifiche, fimbo usije muuwa
    Akitoka bora mche, hapendi kukaribiwa
    Usijifanye macheche, kutaka kumraruwa
    Atakudhuru muwache, ana moto usojuwa

Maher(Unique)

 

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet