.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Unaniumiza Moyo

 

Related links

Unaniumiza moyo

 Date: 1 March,  2003

  1. Umenipa mtihani, mgumu kuelezea
    Sirahisi asilani, naogopa kutelea
    Lakini nifanye nini, sina njia kurejea
    Nakuomba niamini, sidhani najitetea


  2. Sinacho chakukuficha, ikawa siri moyoni
    Kila jambo nimeacha, umenitia mbioni
    Nakesha usiku kucha, siyandoto niamini
    Sina nilipokuwacha, nakuwaza mwafulani


  3. Usisikize ya watu,wala rai sichukuwe
    Watakuwambia kitu,ujiudhi uchukiwe
    Laukweli sina mtu,nasitaki ila wewe
    Iwe miaka mitatu,tasubiri unijuwe


  4. Unaniumiza moyo,ukisema sikupendi
    Mwenzio hali niliyo,sirudi wala siendi
    Naingoja siku hiyo,naona siku hazendi
    Naogopa watu choyo,kila kizidi kipindi


  5. Ningeweza kufunguwa,ukapenya fuadini
    Ukasoma nakujuwa,kilichondani moyoni
    Wallahi ningepasuwa,kifuwa vipande chini
    Ikawa yetu muruwa,kapata yako hanini


  6. Pokea yangu ahadi,iko siku itafika
    Dhamiri zetu tasudi,mikononi takuweka
    Na uliko sibaidi,Mungu akishaandika
    Tuvute zetu nyuradi,milango itafunguka

    SALMA KHAMIS (CHAMA).

 

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet