.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

CHEMSHA BONGO-KWENYE UWANJA WA MASHAIRI

 

Related links

CHEMSHA BONGO-KWENYE UWANJA WA MASHAIRI

Date: 3 July, 2003

  1. Kaziye ni kubwabwaja, asemayo hayajuwi
    Kuwakuza wasohaja, simashina si matawi
    Harufu chenza kangaja, sivipofu si visiwi.


  2. Kashika kuwasafisha, choo harufu waridi
    Kutwa atuhamakisha, kuwa yeye ni shahidi
    Nyimbo zake zisokwisha, za tambuu na magadi.


  3. Twaelezwa yalofanywa, machoni hatuyaoni
    Yako tunayoyajuwa, mauwaji ya mitoni
    Na heshi kutusumbuwa, nakututia huzuni.


  4. Yalopita ni mshindo, kusahaulika vigumu
    Yalopita kama nyundo, wakumbuka walasumu
    Yalopita si magendo, uovu wamwanaadamu.


  5. Muumba tupe imani, tusahau ya zamani
    Tumegeuka manyani, twaninginia mitini
    Kutwa tuko vichakani, huu kwetu mtihani.

Hashil S. Hashil

 

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet