.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Bure Sinikadhibishe

 

Related links

Bure Sinikadhibishe

Date: 19 August, 2004

  1. Bure sinikadhibishe, kunitia uongoni
    Wala sijibabaishe, mimi nimekuoneni
    Katu sjikurupushe, mekukuta mikononi


  2. Nyendo zako mezijua, nalibaini zamani
    Juhudi nikachukua, kuitafuta yakini
    Sasa nimekutambua, kama wewe ni Khaini


  3. Haya zimekuondoka, ukasahau hisani
    Huruma zikakutoka, wema usiuthamini
    Leo unababaika, unajuta kitu gani


  4. Wallahi nakuapia, umejitowa thamani
    Kwa mbaya zako tabia, na wingi uhayawani
    Uzuri wako zulia, makazi yako ni chini

Kiitikio:

  • Ni bure hiyana yako, ubaya kunifanyia
    Nimempata mwenzako, mwenye sifa na tabia

Shairi la Ahmed Khamis Al Barwani

Limeletwa na Maher Fundi

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet