.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Chemsha Bongo

 

Related links

Chemsha Bongo

Date: 19 August, 2004

  1. Wenye nogwa tuko wengi, ukimkwaa kiyama
    Hujibadilisha rangi, kinyonga awekwa nyuma
    Wala hawavuti bangi, mikasa yao nakama.

  2. Twendako kuna dharuba, tujizatiti kikweli
    Hakuhitaji mahaba, tujifanye ziraili
    Maneno yawe ya mimba, muwasho wa pilipili.

  3. Ccm muflisi, wakijuacho fitina
    Nyendo zao kama fisi, wakipatacho wavuna
    Wapinzani ni waasi, wao ndio waungwana.

  4. 2005 songombingo, mwaka huo wangojewa
    Hata watokunjwa gongo, akili zawa muruwa
    Mwenye macho awa chongo, kumbe anakuchunguwa.

  5. Mfundoni nimefika, nasubiri zenu hoja
    Kijiwe kitakalika, kama twawa ni wamoja
    Aduwi kumualika, musifikiri viroja.

Hashil

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet