.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Msiyoyajuwa!

 

 

 

 

 

 

Related links

Msiyoyajuwa!

Date:  2 June 2004

  1. Mengi yanasimuliwa, juu yangu na mwandani
    Watu wataka kujuwa, mecheza turufu gani
    Naona mwajisumbuwa, hilo haliwezekani
    Wenyewe tumeamuwa, ni siri yetu moyoni
  2. Yanini kujisumbuwa, nyinyi yawakhusu nini?
    Katu hamtoaguwa, mutabakia kudhani
    Yeye amenichaguwa, kwake sina mpinzani
    Namimi nimeridhiwa, nimezama siutani
  3. Moyoni memchukuwa, kanijaa akilini
    Anang,ara kama juwa, lililopo utosini
    Haku wakumpikuwa, na mwenyewe kabaini
    Munapita kwenye guwa, tumeshavuna zamani
  4. Ni bure mutapagawa, sisi hatuwezekani
    Hata mukijihashuwa, ndani yetu hamuoni
    Sisi tumejaaliwa, kwa uwezo wa manani
    Mchele hauna chuwa, sasa mwadondowa nini?

 

Chakupewa

Msiyoyajuwa!

Date:  3 June 2004

  1. Ewe uloghaibani, salamu menifikia
    Umewapoza mwandani, siri waifatilia
    Niwajibu jibu gani, nyoyo zao kutulia
    Hii siri ya moyoni, kwa vipi nitawambia
  2. Nibora ungeimeza, wakabaki kuumia
    Sasa umewachokoza, wawatangisha nanjia
    Kwani wanibembeleza, nipate kuwafunilia
    Kwa kipi kilokupoza, moyoni ukanitia
  3. Kwako nimesharidhika, sina budi kuwambia
    Meniweka mewekeka, nyonda kunitimizia
    Wabaki kuhangaika, kwa dhana zilowangia
    Siri nimeifutika, nyondani kuifungia
  4. Kaditamati mefika, sina la kuwaambia
    Nakunja wangu mkeka, kitanda nakimbilia
    Nnamuomba rabuka, sitoke wakulingia
    Wapite kuhangaika, nasie tumetulia

 

Miminae

 

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet