|
|
NINI KOSA LANGU ?
Date: 14 July, 2004
- Ewe uliye mwandani, salam yangu pokeya
Nisikize kwa makini, moyo kunisabiliya
Nataka wako undani, upate nisaidiya
- Tumetokana zamani, hasidi wakiumiya
Ukinipa ya moyoni, na thamani kunitiya
Kimekugeuza nini, mara menigeukiya
- Kosa langu kitu gani, kheri kunitamkiya
Usipite vipembeni, lana kunipakaziya
Alokamilika nani, katika hii duniya
- Haitakuwa vibaya, iwapo utanambiya
Kama nimekukoseya, ni radhi kukwangukiya
Wala sitoona haya, kwako wewe mardhiya
MIMINAE
NINI KOSA LANGU ?
Date: 18 July, 2004
- Mwendani sinishtaki, Likupatalo nyamaza
Mimi sitokushiriki, wala sitokuuliza
Kula mtupa tariki, hawachi kujipoteza
Asietaka kufunzwa, hasalimilki na jambo.
- Nalikwambia kitambo, mwendani wangu sikiza
Sicheze na Mawi mambo, ukanambia tacheza
Leo twapigana kumbo, kula twendapo husoza
Asietaka kufunzwa, hasalimiki na jambo.
- Ulijifanya mwekevu, kula jambo waliweza
Kwa kutamania nguvu, akili ukapoteza
Leo yamekua wavu, tatizi mekutatiza
Asietaka kufunzwa, hasalimiki na jambo.
- Nalikwambia latisha, ukapinga tangu mbele
Na leo limekutwesha, vumilia vile vile
Mwiba wa kujitonesha, mtu haambiwi pole
Asonyooka milele, hasalimiki na jambo.
- Undani wangu ni huo, nao sio mwegineo
Nimekujulisha hayo, kurekebisha ni kwako
Dunia si tegemeo, huzamisha wenye vyao.
Asietaka kufunzwa, hasalimiki na jambo.
Abdul
|