|
|
WEWE NI PUMZI ZAKE
Date: 30 September, 2004
- Anahitaji mapenzi, na deko lako kupewa
Kwa hanini umuenzi, roho ipate kutuwa
Umpunguze majonzi, alonayo yasopowa
Bila ya wewe hawezi, kuishi akawa sawa
- Wewe ni pumzi zake, uhai ulobakia
Hana pengine ashike, kwako yeye maridhia
Simuadhibu muweke, mwenzio anaumia
Lizuwie chozi lake, asichukie dunia
- Tepe tepe hajiwezi, kesha umem'maliza
Anasema wazi wazi, hafichi anatangaza
Si maskhara hachezi, ndani yana muunguza
Anachoomba ulezi, pendo lenu kulikuza
Maher Fundi
|