|
|
KIUMBE HASARIFIKI
Date: 23 January, 2005
- Huyo kachanganyikiwa, hana mbele hana nyuma
Mwenyewe nguo kavuwa, kwenye hadhara ya umma
Kaishiwa kachachiwa, namuonea huruma
Achekwa akejeliwa, kila akijitutuma
- Azurura kila njia, mambo yamemsakama
Asumbuka na dunia, wateja wamemhama
Apita kukamatia, aibu mji mzima
Muflisi wa tabia, kila mtu amsema
- Alipopewa shubiri, yeye kachukua pima
Alijidhani hodari, kutamba na kunguruma
Kumbe watu wamnyari, kimya wanamtazama
Keshamaliza safari, amekwisha kadi tama
- Kiumbe hasarifiki, Wallahi bora mnyama
Ni thakili habebeki, saliti wa kila jema
Makuhuluki mnafiki, mwishowe hana salama
Stahili mzandiki, radhi zinamuandama
KIITIKIO
Kiumbe hasarifiki, saliti wa kila jema
Jaza yake mzandiki, radhi zinamuandama
Shairi: Saleh Barkey - 16th August, 1997
Limeletwa na unique
|