.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

NYUKI

 

 

 

 

 

 

Related links

NYUKI

Date: 11 September, 2005

Shairi hili la NYUKI nililetewa na Sk. Khamis bin Nassor Al-Nabhani Mola amrehemu kabla ya kufariki kwake. Ameeleza kua mtungaji wa shairi hili ambae ni mshairi wa enzi zake za zamani hakutaka jina lijulikane na wengi na ndio maana hakulieneza kwa watu wengi. Kabla kufariki kwake Sheikh Khamis, Mola amrehemu, alisema ndio maana hivi sasa katika kisiwa cha Pemba utalikuta shairi hili kwa watu wawili nao ni yeye mwenyewe na Sarhan bin Matar.

  1. Mambo ya juzi Selemu, Amma hayawasifiki
    Hicho ni kisa adhimu, Wala mwerevu hacheki
    Waarabu mahashumu, Vidudu kuwahiliki
    Kumbe kukimbia nyuki, Mashekhe mbio ni bora

  2. Vita vya nyuki vigumu, Nakhiyari vya bunduki
    Waja hawana salamu, Wala hawanasihiki
    Wakitokea karamu, Kataani hailiki
    Kumbe kukimbia nyuki, Mashekhe mbio ni bora

  3. Tulitaraji wageni, Saa mbili hawazuki
    Wote wako mibiyeni, Wanazama kama diki
    Baadhi ya ariyani, Libasi haziwaviki
    Kumbe kukimbia nyuki, Mashekhe mbio ni bora

  4. Walinipita kikundi, Shekhe Salimu na Muki
    Wakaingia kwa fundi, Kilango hakisinduki
    Wakaumwaga mtindi, Na majungu ya samaki
    Kumbe kukimbia nyuki, Mashekhe mbio ni bora

  5. Na qadhi bwana Nasoro, Musemae hashituki
    Akipata uchochoro, Uchanja haualiki
    Alienea michoro, Kwa mashimo na masiki
    Kumbe kukimbia nyuki, Mashekhe mbio ni bora

  6. L-akhi bin Majidi, Musemae hakunjuki
    Ajidai majuhudi, Enda kwa punda hashuki
    Dharura ikimbidi, Enda mbio hashindiki
    Kumbe kukimbia nyuki, Mashekhe mbio ni bora

  7. Bwana wa Kizuiyani, Mwajuwa simdhihaki
    Ejitupia majani, Wala hayamfuniki
    Nilimkuta njiani, Unaziba muiliki
    Kumbe kukimbia nyuki, Mashekhe mbio ni bora

  8. Aidha bwana wa Tungwe, Ni mrembo haondoki
    Leo pakilia n'gongwe, Kataa hapamueki
    Alitambaa na bonde, Hadi rasi ya pichiki
    Kumbe kukimbia nyuki, Mashekhe mbio ni bora

  9. Vilikutana vipungo, Kupungwa bwana Lemki
    Nyuki kaipa mgongo, Wala hakutaharuki
    Na vile kutoa shingo, Akenda kama hataki
    Kumbe kukimbia nyuki, Mashekhe mbio ni bora

  10. Tamma bin Ibrahimu, Kila epiga falaki
    Esema hayatadumu, Efanya kama hataki
    Ilishtadi zihamu, Pasiwe alamsiki
    Kumbe kukimbia nyuki, Mashekhe mbi ni bora
  11. Limetwa na Saleh Barkey

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet