Date: 13 December, 2005
Kwa wale
wapenzi wa sanaa hii ya urari wa vina, na muwala wa beti na mishororo
y! ake, huu ni utungo wa kiroho na kimaanawi. Tafadhalini natuusome
kwa kituo.
************
MWISHO NIMEFIKA
Mwangi
unagonga, sikioni mwangu, mja kuniita, natika labeka.
Yule
anopanga, kunondoa pingu, kutoa utata, nuru nawirika.
Kaja njiwa
manga, zanawiri mbingu, kheri kuipata, kuusha mashaka
Ni Allah
wangu Rabuka.
Kaondoa
wingu, akili burudi, twabiki fiili, ndipo taokoka
Busitani
yangu, kajaza waridi, nazo mbawa mbili, kanipa Rabuka
Udhaifu
wangu, mkubwa shitadi, kanipa akili, iwe kuongoka
Ni nani Wako
mithili?
Kanifunza panda, paa uenende,
fika kileleni, twii Mtukuka
Ni wangu
uwanda, napepea nende, Kwake Rahmani, nifike haraka
Nechoka
kuranda, nemaliza konde, hikwama kingoni, mwisho nimefika
Kwa Nuru
yangu samawi.
Nalijidanganya, hajipurapura, nikajipumbaza, eti sina shaka
Yakanikanganya, kuniparapara, yakanichakaza, nikafadhaika
Mja
kunifinya, dunia tambara, limeniburuza, yameshanifika
Mwokozi
unasi ameniokoa.
Nyuma sendi
tena, Kwake nimesaki, sikutaki tena, dunia mashaka
Niko hai
tena, ni kwa Mmiliki, moyo sifi tena, nimeshaokoka
Sinache
Rabbana, mja tahiliki, nekusaka sana, mwisho nimefika
Ni Wewe tu
Rabbuka.
************
Ahmed Rashid