.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Nyumbani ni Nyumbani!

 

 

 

 

 

 

Related links

Nyumbani ni Nyumbani!

Date: 28 May, 2006

  1. Nikikumbuka nyumbani, hukaa najinamia
    Hujiona maskini, ingawa navumilia
    Ukweli siko rahani, rohoni ninaumia
    Ugeni si kitu chema, maskini mtu kwao

  2. Nyumbani hakurudiki, watu wamekuvamia
    maisha yako ya dhiki, wamrima watanua
    Uhuru hausemeki, woga umetujalia
    Ugeni si kitu chema, masikini mtu kwao

  3. Ninakumbuka udogo, tulivyo tukitulia
    Hakukuwa na vichogo, waungwana weenea
    hatukuona mgogo, kahawa kujiuzia
    Una karaha ugeni, masikini mtu kwao

  4. Ninaporudi kazini, kucha ndani hubakia
    computer ukumbini, na TV kwangalia
    macho hufika huoni, mionzi mekujalia
    Masikini mtu kwao , ugeni si kitu chema

  5. Ibada ni mtihani, swala hujipitilia
    Darasa misikitini, hadithini hubakia
    Watu hawajali dini, dunia wafikiria
    Ugeni si kitu chema, masikini mtu kwao

  6. Iko siku tutarudi, sisi ni wavumilivu
    Na wasomi ikibidi, waje waongeze nguvu
    na mola atatuhidi, hatutofanya maovu
    Ugeni si kitu chema, masikini mtu kwao.

Anonymous 282

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004-2006 Zanzinet