.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Mumetusaliti!

 

 

 

 

 

 

Related links

Mumetusaliti!

Date:  10 January, 2006

  1. Wambie wambie, twaafiki, uliyotwambiya
    Kawahutubie, wanafiki, wasio na haya
    Sema wasikie, yastahiki, kuwapasuliya
    Walimwengu tupo twasikiya!
  2. Kila msaliti, na yeyote, anayewasifu
    Na akawasuti, sifa zote, za watakatifu
    Huyo afiriti, si lolote, ana hitilafu
    Sio muungwana ni mdanganyifu!
  3. Iwe ni Padiri, wa dhehebu, linalotajika
    Shekhe wa kadiri, kwa vitabu, alivyovishika
    Hebu tafakari, kwa karibu, anayotamka
    Wake umahiri unatia shaka!
  4. Wasomi kalamu, na wenzao, walionyamaza
    Hutaka zidumu, kazi zao, kwa kuwapongeza
    Hawa madhalimu, basi nao, bora kupuuza
    Na ikibidi kuwaapiza!
  5. Na hao wengine, waadhama, uliowataja
    Zao dane dane, sio njema, Pemba na Unguja
    Damu kwa matone, kwa majuma, kwetu ikivuja
    Kwao wao si kioja!
  6. Mwisho sina budi, kuungana, na wetu malenga
    Kwamba Mohamedi, vyako vina, umevikuunga
    Wewe si baidi, tunga tena, nyoyo ukikonga
    Ndipo utaona raha ya kutunga!

 

Kassim O. Ali

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004-2006 Zanzinet