.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

NCHA YA KISU KOONI !

 

 

 

 

 

 

Related links

NCHA YA KISU KOONI!

Date: 09 March, 2006

  1. Nakupeni yalo ndani, ya ng'o hatukubali
    Sio ya mkahawani, au baoni ya kweli
    Mazito yako kooni, kwao ni kitendawili
    Baba fimbo mkononi, watoto na wafadhili

  2. Si uvumi pata shika, shinani Kisiwanduwi
    Ngumi mtu chupa ruka, wachungu huwaelewi
    Mvute nguo chanika, walivyo kama wachawi
    Makonde ya mwangaruka, na nyimbo hatuitowi

  3. Kaja kutoka mrima, mdogo wa baba yao
    Kupatanisha hasama, ya wawili chombo chao
    Kwaheri chenda mrama, zimekwisha zama zao
    Haya maneno mazima, shikeni yawe ni tao

  4. Hazitimu siku tatu, ikafata msijue
    Si ya kupigwa upatu, wala beni mtambue
    Wevi warudisha chetu, haki yetu tuchukue
    Tuijenge ngome yetu, na mazuri tuamue

Maher ( Unique )

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004-2006 Zanzinet