|
|
NA SISI TUMECHOKA!
Date: 02 April, 2008
- Nakupa yangu pongezi, Abuu Shani kutujuvya
Mawazo yako mapenzi, Zenjibari kutukuka!
- Kwa haya uliyosema, yatupasa kukwambia
Ni ya wingi wa rehema, kwa wakati kuwadia!
- Na hakika umeona, pa ukweli kupangia
Sefu naaje kushona, yake nguo kuchangia!
- Salimini atapona, macho yake kutangia
Pale Jumbe aliona, imani kumjilia!
- Mwinyi pia ana kona, ya mpira kupigia
Na Bilali hatofonya, kwenye kheri kuingia!
- Haya maneno kutona, si mazito kusikia
Ni yetu sote kuponya, kuchanganya zetu nia!
Salim Himidi
|