.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

NI MOYO AU AKILI!

 

 

 

 

 

 

Related links

NI MOYO AU AKILI!

Date: 23 January, 2008

  1. Nauliza mujuao, Mulio na nyingi fani
    Watu na elimu zao, Magwiji na Magogeni
    Nimekwama hadi leo, Mebaki mushkelini
    Unaopenda ni moyo, Au akili kichwani?
  2. Wengi niwasikiao, Kila kona mitaani
    Husema mioyo yao, Meingia mapenzini
    Sisikii wasemao, Yamengia akilini
    Naulizia Ni Moyo, Au akili kichwani?

  3. Hodari wasifiwao, Madarasa na Shuleni
    Hutajwa akili zao, Moyo haujulikani
    Naufikiria moyo, Hapa una kazi gani
    Ndio kweli upendao, Au akili kichwani?

  4. Moyo ndio upigao, Damu ikenda mwilini
    Kama tasimama leo, Ni kuzikwa kaburini
    Nakubaliana nao, Hapo sina upinzani
    Unaopenda ni moyo, Au Akili kichwani?

  5. Fikira na mengineyo, Hapo ndio mtihani
    Kila Ucha na Uchao, Siuoni ulingani
    Sijui undani wao, Wamekusudia Nini?
    Unaopenda ni moyo, Au akili kichwani?
  6. Sio watu Peke yao, Bali hata vitabuni
    Kila ncha uendayo, Ulaya na Arabuni
    Kauli ndo hiyo hiyo, Moyo kitiwa kinywani
    Naulizia ni moyo, Au akili kichwani?

  7. Masuali ndio hayo, Jibuni Mlo Makini
    Msikimbilie mbio, Kuna mteno wa ndani
    Kuyajua yasemwayo, Kunataka Umakini
    Unaopenda ni Moyo, Au Akili kichwani?

  8. Niliyouliza hayo, Kabisa sio utani
    Mimi nina shida nayo, Niondoke utatani
    Ka Bakari na wenzio, Jama Nisaidieni
    Naulizia ni moyo, Au akili kichwani?

Amour Rashid

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet