.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

RISALA KWA MAALIM HASHIL!

 

 

 

 

 

 

Related links

RISALA KWA MAALIM HASHIL!

Date: 30 April, 2008

  1. Maâlim Hashil sogea, leo tupate ongea
    Haidari kachochea, Wakomoro kupokea
    Kwa haya yalotokea, haki yako kutetea!

  2. Kwa kweli umebobea, na haya yakuelea
    Bob Denard kutulengea, mamluki kutupondea,
    Komoro yateteketea, hapana pa kusemea!

  3. Haya yote nakwambiya, Faransa imepania,
    Komoro kuangamia, faida kujipatia
    Mayotte kuikalia, msingi wa hayo pia!

  4. Hawa kina Haidari, wao kweli mahodari
    Ngazija si kachumbari, si nguru wala jodari
    Wafanyeje ya fahari, nyama imetaghayari!

  5. Kwa leo nakuachia, ujue si rakhisia
    Vituko vya Komoria, ukoloni jahiliya
    Jeshi hilo Afrikiya, ni sawa na mabandia!

  6. Mwisho hapa tunaweka, wino na kalamu pia
    Hatuna pakueleka, si kichochoro si njia
    Tumeshindwa na kufyeka, seuze pa kufagia!

  7. Wajibu wako Maâlim, kufunguwa yetu macho
    Usingojee ya Muusim, kufichua ujuwacho
    Hata ikiwa ni Muslim, usiche jicho la kwacho!

salim Himidi

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet