|
|
SIULUMBI MULUMBAO!
Date: 09 January, 2008
- Ndimi mgeni wa Numbi, mwenyeji kale 創okuwa
Nijili kwenu waambi, kuzinga la kuambiwa
Bali hakuta ulumbi, nami ukanishituwa
Na nilipouchunguwa, haona ni wa vitimbi.
- Ging段ngi ya Waging段ngi, si ya miye mtolewa
Nami nacha nena mengi, bawabu akanitowa
Lakini hayanitwangi, maneno yanotumiwa
Kulumbana kwa vifuwa, si ulumbi wa Ging段ngi.
- Waging段ngi kwa ulumbi, ni kazi yenu najuwa
Bali sio ujigambi, wa wengine kuumbuwa
Kwamba mtamba hatambi, asikucha kutambiwa
Mbona nyie mwacheuwa, au mushashiba tumbi?
- Nasi tuli Waging段ngi, wa kutolewa vikowa
Tukalumbana kwa mingi, bali lugha twechaguwa
Mbona nyie hamutungi, mwaumba mukiumbuwa?
Kwa hivi munabomowa, ndugu zangu hamujengi.
- Lau kweli mu walumbi, lumbanani kwa satuwa
Musilumbane kwa kambi, na pande pande mukawa
Agambapo mjigambi, ujuwe hajajijuwa
Kwamba lau ajijuwa, mwenye gambo hajigambi.
- La urongo silirongi, madharaye nayajuwa
Nawe ola Mging段ngi, 壮ingoje ukalolewa
Kwamba zipo siku nyingi, zako weye hapa kuwa
Vipi ulomshushuwa, akaja kuwa ni mwingi?
- Ulumbi wa ujigambi, na kujipiga kifuwa
Mlangoni pa Ging段ngi, si jambo la kusifiwa
Uonwe kuwa ni dhambi, na kharamu yenye dowa
Nami ninawazinduwa, mukome huu ulumbi!
Mohammed Ghassani
SIULUMBI MULUMBAO!
Date: 10 January, 2008
- Al Akhi mshairi , baswiri muona mambo
Katu si yangu dhamiri , kukupiga kwa vikumbo
Uliyonena hariri , tuyatakayo kitambo
Wagange watagangika , Gin'gingi nawe ni mwako
- Nduguyo akinaswa , kwa fitina kuwa chambo
Huraiwa na kuaswa , asizidi kwenda kombo
Kuongozwa si kukoswa , nasaha ni chema chombo
Wagange watagangika , Gin'gingi nawe ni mwako
- Walumbao yasolumbwa , watuumiza matumbo
Awali ndivyo kuombwa , kutaradhiwa kwa nyimbo
Mwishowe sawa kugombwa , washikiwe hata fimbo
Wagange watagangika , Gin'gingi nawe ni mwako
Saleh M. Barkey
|