.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

UKUMBI UMEDORORA!

 

 

 

 

 

 

Related links

UKUMBI UMEDORORA!

Date:  03 January, 2008

  1. Ukumbi ulidorora, sasa umechangamka
    Tulete yalio bora, tusije kuchawanyika
    Tusitembeze bakora, kuja kuchanja nyika
    Ukumbi huu imara, watu hawatabanduka

  2. Zitoke kila idara, habari zikitendeka
    Wala isiwe kafara, ukumbi kumahanika
    Yataka nyingi busara, walolala kuamka
    Ukumbi huu imara, watu hawatabanduka

  3. Tusionyeshe hasira, pale tunapoamka
    Tulete nyingi tijara, jua kupambazuka
    Tusifanye masikhara, ukumbi kuchakarika
    Ukumbi huu imara, watu hawatabanduka

Ali Abdulkadir

UKUMBI UMEDORORA!

Date:  03 January, 2008

  1. Ukumbi wetu ni bora, si wa kutanga na nyika
    Hauhitaji bakora, wala kadi kualika
    Risala zaja tikrara, soma bila ya kuwika
    Sidhani watabanduka, wasemao wadorora

Professor Ibrahim Noor

UKUMBI UMEDORORA!

Date:  03 January, 2008

  1. Kweli msemayo ni kweli, Mwinyi Ibrahima na Ali
    Kwa yote haya yakifeli, sote kukosa yetu mali
    Hasara si za makubeli, na kabwela hana amali!

  2. Hapa pia natawakali, tangulize yetu imani
    Kwani kidogo si a'kali, kukutana sote jamani
    Zendjibari ni Biriyani, si mseto wa Makuhani!

  3. Mwasemaje nyi wanawari, wenye hii njema Bustani?
    Kudorora si afu'ali, za kutengana na wandzani
    Huyisha yetu Zinjibari, ewe Mola wa Manani!

  4. Hapa tamati nastakari, yangu tamaa kuvumbika
    Na wallahi sijakubali, kuwa Jogoo hatowika
    Kiza hufuatwa na nari: yuwapi atakae pinga?

Salim Himidi

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet