.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

WAPINZANI WATOKA BUNGENI!

 

 

 

 

 

 

Related links

WAPINZANI WATOKA BUNGENI!

Date: 10 April, 2008

  1. Maalim wangu Hashili, Kinara fundi mwanana
    Mawazo yako kukiri, ni fimbo ya Subuhana
    Yenye wingi wa akili, kwa marefu na upana!

  2. Kwa marefu na upana, lazimu wewe utete
    Wala si kwa kutukana, hayo sio ya upweke
    Watapowafikiana, Zanzibar kwenda kidete!

  3. Zanzibar kwenda kidete, ni mambo kuyafahamu
    Mfunga watu Kikwete, yadhibiti mahakimu
    Tusije kuwa viwete, kushindwa na mabuhamu!

  4. Kushindwa na mabuhamu, ni sawa na kwendwa choo
    Vinyama na wanadamu, sote wana wa kondoo
    Tumuandame kwa hamu, Kubeli la Bagamoyo!

  5. Kubeli la Bagamoyo, ndie mwenye kukithiri
    Amali za matokeo, kupunguza pilipili
    Mapenzi yetu ya leo, yatupasa tufikiri!

Salim Himidi

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet