.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

JAHAZI !

 

 

 

 

 

 

Related links

JAHAZI!

Date: 18 May, 2006

  1. Liembete na mongoti, tanga kwa lingi shauri
    Hautukuti ukuti, imetuwama bahari
    Hata mai hayavuti, tutapatae bandari?

  2. Ngurudi imeshopoka, mai ngamani hujiri
    Haitaki kuzibika, na hata kwa misumari
    Kuyafua tumechoka , mikono hutuhairi

  3. Tumekosa taratibu , hatuna tena shauri
    Na bandari si karibu , hakupiti manuwari
    Zimetutanda dharubu , metuzunguka khatari

  4. Hatuisi la kutenda , tumeshindwa kufikiri
    Kiza kingi kimetanda , kote kimepija dori
    Ni heri mwamba kupanda , kama hunu utiriri

  5. Hatuna ila Manani , wa kumuomba Jabari
    Atwegeshe nasi pwani , yapokuwa kwa kihori
    Tuokowe Rahamani , waja wako tusitiri

  6. Suwali si la jahazi , hili katika shairi
    Litambuweni wayuzi , mafundi mulo hodari
    Wa mtoni wende mbizi , muzizamiayo duri

Limetunga tarehe 21-3-2002 na Ustadh Mahmoud Ahmed Abdul Kadir (MAU) kutoka Lamu - Kenya.

Limeletwa na Sheikh Saleh Barkey

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004-2006 Zanzinet