.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Kuukomboa Wa'tani

 

 

 

 

 

 

Related links

KUUKOMBOA WA'TANI
(Kutoka Katika FZV)

Date:  25 February, 2005

Utenzi huu ulitolewa katika gazeti la Umoja wa Wazanzibari (Free Zanzibar Voice) mnamo 1968 linaonesha hisia za Mzanzibari mwenzetu akitunadia katika ukombozi wa Wattani wetu, juu ya fahamu yake kuwa Wattani ndio mama yetu. Ni miaka thalathini na saba, yaani tangu 1968; lakini yaliosemwa ni madhubuti na ni kama yamesemwa jana au leo. Hapana shaka Wazanzibari ni wenye uwezo wa kuirejesha Dola yao Huru ya Zanzibar kama ilivyokuwa kabla ya mavamizi ya 1964. Penye nia pana njia.

  1. Wat'ani watoja damu, 'tabibu twapiga hodi
    Hima hima muadhamu, Sinene nenda urudi
    Kukawia ni haramu , na kutoa huna budi
    Kwani hii ni Jihadi, kuugomboa Wat'ani
  2. Mwanao ayayatika, mama muwahi waladi
    Mwanao atakutoka, usipofanya juhudi
    Kilio chake pulika , kinapasua fuadi
    Isaidie Jihadi , ya kugomboa Wat'ani
  3. Mamiyo alokuzaa , ni mpweke na wahedi
    Kakuzaa kwa fazaa , na dhiki mno shadidi
    Zengea yake ridhaa , ipate ya Wadudi
    Kwani hiyo ni Jihadi , ya kugomboa Wat'ani
  4. Na baba yako mwanangu, na pia na wako jadi
    Usiwatie matungu , hata ukapita hadi
    Kumbuka zama za tangu , uwache yako inadi
    Wajibu wako Jihadi , kuugomboa Wat'ani
  5. Mama watoto nyumbani , alozaa auladi
    Mkapishana yamini , kukidhi wenu muradi
    Wote hao ni Wat'ani , na hao ndio biladi
    Unga mkono Jihadi , tuugomboe Wat'ani
  6. Na nchi yetu tukufu , si maiti ni shahidi
    Kwani shahidi si mfu , kila siku ni jadidi
    Umma hai mashe khofu, walo mbali watarudi
    Wataingia Jihadi , kuugomboa Wa'tani

Mzanzibari
1968

Umeletwa na Farouk Amour

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet