.

Welcome to Zanzinet Swahili Poems

Where Swahili matters!

Ulimi

 

Related links

             Ulimi!

Date: 26 August, 2004

  1. Ulimi ni tamu, ukiutongowa
    Wa ama ni sumu, ya kusongonyowa
    Uyuwe fahamu, na mwiso huuwa

  2. Ni nyama laini, haina mfupa
    Njema kwa lahani, Mola ametupa
    T'unu ya thamani, usio mshipa

  3. Utatuma wema, kwa wako wendani
    Ndugu kukugema, na kuya nyumbani
    Lakukusukuma, halipatikani

  4. Kwa baba na mama, kuwekwa paani
    Utakuwa mwema, na kwa majirani
    Kuyuwa kusema, ni usulutwani

  5. Wasokufahamu, wauze ni nyani?
    Wafanye hamumu, waje masikani
    Na wakuhishimu, wawe wa nyaoni

  6. Swarifu hisani, uwekewe mbeko
    Kwa nde na ndani, na kwa wat'u wako
    Daraja ya shani, towa shaka ndako

  7. Hutowa pangoni, nyoka kaja kwako
    Katoka waani, asiche zituko
    Yako ulimini, mema matamko

Limeletwa na Saleh Bakey

Mtungaji : Shaha: Ahmed Sheikh Nabhany (Mombasa - Kenya)

  About Us | Zanzinet Home | Contact Us | ©2004 Zanzinet